Sababu ndege za Kenya kuruhusiwa kutua Tanzania

September 16, 2020 12:11 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya Kenya kuondoa sharti la raia wa Tanzania kukaa karantini kwa siku 14 wanapoingia nchini humo.
  • Sasa wasafiri wa nchi hizo mbili wako huru kutumia ndege za Kenya. 

Dar es Salaam. Unaweza kusema ni kicheko kwa wasafiri wanaotumia mashirika ya ndege ya nchini Kenya likiwemo la Kenya Airways, baada ya Serikali ya Tanzania kuruhusu ndege za nchini hiyo kutua nchini. 

Hatua hiyo imekuja baada ya Kenya kuondoa sharti la raia wa Tanzania kukaa karantini kwa siku 14 wanapoingia nchini humo ambalo lilikuwa limekwa awali ili kujikinga na Corona.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Johari Hamza katika taarifa yake iliyotolewa leo (Septemba 16, 2020) amesema kutokana na kulegezwa kwa masharti hayo, ndege za Kenya zinaruhusiwa kutua tena nchini.

Johari amesema ndege zote za mashirika ya Kenya za Kenya Airways, Fly 540 Limited, SafariLink Aviation na AirKenya Express Limited zinaweza kutua katika viwanja vya ndege vya Tanzania kwa muda wote.

Amesema tayari wameitaarifu Mamlaka ya Usafiri wa Anga Kenya kuhusu kuruhusiwa kwa ndege hizo.


Soma zaidi:


Julai 31 mwaka huu, Serikali ya Tanzania ilibatilisha kibali cha ndege za Shirika la ndege la Kenya (Kenya Airways) kutua nchini ikiwa ni majibu dhidi ya uamuzi wa Serikali ya Kenya kutoiweka Tanzania katika orodha ya nchi ambazo raia wake wangeruhusiwa kuingia Kenya kuanzia Agusti mos bila kukaa karantini. 

Hata hivyo, jana Septemba 15, Kenya imeondoa sharti la Watanzania kukaa karantini siku 14 kabla ya kuruhusiwa kuingia nchini humo. 

Muda mfupi baada ya anga la Tanzania kufunguliwa kwa ndege za Kenya, shirika la ndege la Kenya Airways limesema litaanza safari zake za kwenda jijini Dar es Salaam kuanzia Jumatatu Septemba 21. 

“Ndege yetu ya kwanza kwenda Dar es Salaam itakuwa Jumatatu Septemba 21, ambapo tutakuwa na safari ya asubuhi na safari  ya pili itakuwa Septemba 23. Safari za kwenda Zanzibar zitarejea Septemba 26 kwa safari tatu kwa wiki; Jumatatu, Jumatano na Jumamosi,” imeeleza Kenya Airways katika taarifa yake iliyotolewa leo.

Hiyo siyo mara ya kwa nchi hizo mbili kuingia katika mivutano ya kibiashara, licha ya kuwa zimekuwa zikitegemeana katika shughuli mbalimbali za kiuchumi. 

Kenya inawakilisha asilimia 4.3 ya mauzo yote ya nje ya Tanzania na asilimia 4.1 ya manunuzi yote ya Tanzania kutoka nje ya nchi. 

Inaelezwa kuwa zaidi ya kampuni 529 za Kenya zinaendesha biashara zake nchini Tanzania na zimewekeza zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 1.7 (takriban Sh39.5 trilioni) na kutengeneza ajira kwa Watanzania zaidi ya 56,260.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV