RC Mwanza apiga marufuku mikusanyiko isiyo ya lazima

July 20, 2021 1:19 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Amesema hiyo itasaidia kupunguza maambukizi ya Uviko-19.
  • Aagiza watu kuvaa barakoa, kunawa mikono.

Mwanza. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Roberth Gabriel  amepiga marufuku mikusanyiko ya vikundi mkoani Mwanza visivyokuwa na ulazima ili kujikinga na ugonjwa wa Corona (Uviko-19) wimbi la tatu.

Gabriel aliyekuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa leo Julai 20, 2021, amesema katika kuendelea kujikinga na ugonjwa huo kuna mambo ya kufanyia marekebisho ikiwa ni pamoja na utoaji elimu pamoja na suala la ufuatiliaji.

Katika suala hili la ufuatiliaji, kiongozi huyo amesema hakuna ulazima wa kuwepo kwa mikusanyiko isiyo ya lazima na katika maeneo yanayowakutanisha watu kama kanisani, misikitini au sokoni watu wahakikishe wanavaa barakoa.

“Niwaombe viongozi wa wilaya, tarafa na kata kuhakikisha wanafanya ufuatiliaji kwenye maeneo hayo, mtu anapoenda sokoni hakikisha kuna ndoo za kunawia mikono na amevaa barakoa  ili wakati wanapobadilishana fedha isiwepo namna inayoweza kusababisha maambuki,” amesema Gabriel

Ameagiza viongozi wa wilaya kuzingatia utoaji wa vibali vya kufanya mikusanyiko kwenye maeneo yao huku akiweka ulazima uvaaji barakoa maeneo mbalimbali kama misibani, sokoni na kwenye ofisi za  serikali kabla ya kumhudumia mtu.

“Mwanza ni mkoa hatuwezi kucheza na maisha ya watu ni lazima tuzingatie maelekezo na kutoa elimu ya watu kujikinga na kupeana nafasi,” amesema.

Pia ameagiza kuwepo kwa vifaa vya kunawia mikono na vitakasa mikono kwenye maeneo ya shule na kama hakuna wahakikishe wanaweka huku wananchi wakitakiwa kuendelea kujikinga na kuchukua tahadhari.

Anasema wakiendelea na kampeni hii ndani ya miezi mitatu ijayo hali inaweza kuwa tofauti kwa kuwa Mkoa wa Mwanza unatajwa kuathirika na janga hili kuliko mikoa yote Tanzania.

Amewataka wasafiri wasiogope kufika na kuwa wachukue tahadhari, na kwamba matamasha, mikutano ya hadhara  ya kisiasa na mingine itakuja baadaye.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV