Necta: Hatujatangaza matokeo ya kidato cha nne 2022
- Wananchi watakiwa kupuuzia taarifa hizo
- Necta yasema matokeo yatatangazwa muda wowote yatapokuwa tayari.
Dar es Salaam. Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limewataka wananchi kupuuzia taarifa zinazosambazwa mtandaoni kuwa baraza hilo limetoa matokeo ya mitihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka 2022.
Necta imetoa taarifa hizo leo Januari 25, 2023 kupitia taarifa ya Afisa Habari na Mawasiliano wake, John Nchimbi ambapo imejulisha umma kuwa taarifa hizo zinazosambazwa kuhusu baraza hilo si za kweli.
“Baraza linapenda kuujulisha umma kuwa taarifa hizo ni za uongo na zinalenga kupotosha umma na kuleta taharuki,” amesema Nchimbi katika taarifa hiyo.
Soma zaidi
-
Lissu awasili, mamia wajitokeza kumpokea Dar es Salaam
-
Panga pangua ya Rais Samia kwa wakuu wa wilaya hii hapa
Taarifa hiyo imefafanua zaidi kuwa matokeo ya kidato cha nne 2022 yatatangazwa rasmi na baraza hilo kupitia vyombo vya habari muda wowote yatakapokuwa tayari.
Mtihani wa Taifa wa kidato cha nne kwa mwaka 2022 ulianza kufanyika Novemba 14 na kumalizika Disemba 1, 2022 huku watahiniwa 566,840 kutoka shule 5,212 wakisajiliwa kufanya mtihani huo.
Kwa kawaida matokeo ya mtihani wa kitaifa wa kidato cha nne hutangazwa Januari au Februari.
Latest