Mikopo kwa sekta binafsi yapungua Tanzania

March 16, 2021 6:38 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Imepungua hadi wastani wa asilimia 8.6 katika mwaka ulioishia Machi 2020 ikilinganishwa na asilimia 9.6 katika kipindi kama hicho mwaka 2019.
  • Sehemu kubwa ya mikopo hiyo bado inaelekezwa katika shughuli za watu binafsi na biashara.

Dar es Salaam. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesema mikopo kwa sekta binafsi imepungua kidogo ndani ya kipindi cha mwaka mmoja uliopita, licha ya sehemu kubwa ya mikopo hiyo kuelekezwa katika shughuli za watu binafsi na biashara.

Ripoti ya Tathmini ya Uchumi ya mwezi Aprili 2020 (Economic Monthly Review) iliyotolewa na BoT hivi karibuni inaeleza kuwa mikopo kwa sekta binafsi imepungua hadi wastani wa asilimia 8.6 katika mwaka ulioishia Machi 2020 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 9.6 katika kipindi kama hicho mwaka 2019.

“Hii inaashiria kuwa kwa sehemu kuna pesa za kutosha za kukopesha kutokana na hatua mbalimbali zinachukuliwa na Serikali kuimarisha sera za fedha,” inaeleza ripoti hiyo.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa sehemu kubwa ya mikopo kwa sekta binafsi imeendelea kuelekezwa kwa watu binafsi  ambao walipata wastani wa asilimia 30.2 ya mikopo yote ikifuatiwa na shughuli za biashara zilizokuwa na wastani wa asilimia 17.7. 


Soma zaidi:


Mikopo inayoelekezwa katika shughuli zote kubwa za uchumi imeendelea kuongezeka, isipokuwa kwa shughuli za hoteli na migahawa, madini na uzalishaji viwandani. 

Hata wakati mikopo kwa sekta binafsi ikipungua, kiwango vya riba kinachotozwa na benki za biashara nacho kimeshuka.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, riba iliyotozwa kwenye mikopo iliyotolewa na benki ilikuwa ni wastani wa asilimia 15.83 mwezi Machi 2020 ikishuka kutoka wastani wa asilimia 17.59 katika kipindi kama hicho 2019.

Wiki hii BoT imetangaza  hatua mbalimbali kupunguza makali ikiwemo kuziruhusu benki kujadiliana na wakopaji wao juu ya urejeshaji mikopo ili kupunguza maumivu wakati huu wa mlipuko wa Corona uliosababishwa kuyumba kwa shughuli za uchumi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV