Mgao wa maji: Majaliwa akagua visima vya dharura Dar

November 14, 2022 3:54 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Oktoba 10, 2022 amekagua visima vya dharura vinavyosafishwa, kufufuliwa na kuunganishwa katika mfumo wa usambazaji maji kwa wananchi na kuagiza zoezi hilo pamoja na uchimbaji wa visima katika maeneo mbalimbali liwe endelevu. Picha | Ofisi ya Waziri Mkuu.


  • Ataka zoezi la uchimbaji na utunzaji wa visima uwe endelevu.
  • Visima 160 kupunguza makali ya mgao wa maji jijini hapa.
  • Mahitaji ya maji ni lita milioni 540 lakini kwa sasa uzalishaji ni lita milioni 300.

Dar es Salaam. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekagua visima vya dharura vinavyosafishwa, kufufuliwa na kuunganishwa katika mfumo wa usambazaji maji kwa wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam na kuagiza zoezi hilo pamoja na uchimbaji wa visima katika maeneo mbalimbali liwe endelevu.

Ukaguzi huo umekuja wakati wananchi wa mkoa huo unaokuwa kasi wakiwa katika mgao wa maji na umeme kutokana na kupungua kwa maji katika Mto Ruvu kulikochangiwa na kuchelewa kwa mvua za vuli. 

Hali hiyo imesababisha usumbufu kwa wakazi hao huku katika baadhi ya maeneo maji yakikosekana kwa zaidi ya wiki tatu mfululizo. 

Majaliwa amekagua visima katika eneo la Tabata Relini na Mwananyamala Komakoma leo Novemba 10, 2022 ambapo ameshuhudia usafishwaji wa visima hivyo pamoja na zoezi la usambazaji maji.

Visima hivyo ni miongozi mwa visima 197 vilivyochimbwa na Serikali mkoani Dar es Salaam ambapo kwa sasa 160 vimefufuliwa na kutoa lita milioni 29.4 kwa siku.

Maji hayo yameunganishwa katika mfumo ili kusaidia kupunguza changamoto ya maji.

Waziri Mkuu ameuagiza uongozi wa Bonde la Wami Ruvu pamoja na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar Es Salaam (DAWASA) waendelee kufanya tafiti kubaini maeneo yenye maji mengi na kuchimba visima na kuyaingiza katika mfumo.

Amewataka wananchi kuendelea kulinda maeneo yote yenye vyanzo vya maji pamoja na kuyatumia vizuri maji yanayopatikana ili kukabiliana na tatizo la upungufu wa maji hususani katika kipindi hiki cha ukame.


Soma zaidi:


Aidha, amesema Serikali imedhamiria kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika mikoa yote nchini likiwemo  jiji la Dar es Salaam kwa kutekeleza kampeni mbalimbali ikiwemo ya kumtua mama ndoo kichwani ili kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma hiyo karibu na maeneo yao ya makazi. 

Mahitaji ya maji katika mkoa huo uliopo katika mwambao wa bahari ya Hindi ni lita milioni 544 kwa siku na uzalishaji maji kwa siku ni lita milioni 520 katika kipindi ambacho kiwango cha maji katika Mto Ruvu kinakuwa katika hali ya kawaida.

 Hata hivyo, katika kipindi hiki ambacho kiwango cha maji kimepungua katika Mto Ruvu uzalishaji wa maji nao umepungua na kufikia lita milioni 300 kwa siku.

Baada ya kuingiza lita milioni 70 kutoka katika mradi wa visima vya wilayani Kigamboni na lita milioni 29.4 kutoka katika mradi wa visima vingine 160 vya jijini Dar es Salaam sasa upungufu wa maji ni lita milioni 145 kwa siku.

Takribani asilimia 40 ya eneo la mkoa halina mtandao wa mabomba ya DAWASA kutokana na uwekezaji mdogo, hivyo kulazimika kutumia visima kama vyanzo vikuu vya huduma ya maji.

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji katika maeneo mbalimbali nchini wizara yake imejipanga kuchimba mabwawa kwa ajili ya uvunaji wa maji ya mvua na kuyaingiza katika mfumo.

“Tutashinda site kuhakikisha maji yanapatikana kwa wananchi,” amesema Aweso.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV