Magari ya kukodi yaongeza gharama za uendeshaji balozi

April 17, 2019 11:17 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imetakiwa kuacha kukodi magari kwa ajili ya shughuli za balozi badala yake inunue magari yake ili kupunguza gharama.
  • Balozi mbili za Tanzania katika miji ya Moroni nchini Comoro na Brasilia (Brazil) katika mwaka 2017/2018 zilitumia Sh87.5 kukodi magari kwa ajili ya shughuli za kila siku za balozi hizo. 

Dar es Salaam. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imetakiwa kuacha kukodi magari kwa ajili ya shughuli za balozi badala yake inunue magari yake ili kupunguza ongezeko la gharama za kukodi magari hayo. 

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Mussa Assad ametoa ushauri huo katika ripoti ya ukaguzi wa hesabu za Serikali Kuu katika mwaka wa 2017/2018 baada ya kubaini kuwa balozi mbili za Tanzania katika miji ya Moroni  nchini Comoro na Brasilia (Brazil) zimetumia Sh87.5 milioni kukodi magari kwa ajili ya shughuli za kila siku za balozi katika miji hiyo.

CAG amesema balozi hizo mbili zimekuwa zikikodi magari kwa ajili ya shughuli za kila siku za balozi, jambo linalokinzana na kanuni ya 84 ya kanuni za Huduma za Umma (Huduma za Nje ya Tanzania) ya mwaka 2016 inayotaka kutoa gari sahihi la uwakilishi kwa Mkuu wa Balozi na gari jingine linatolewa kwa ajili ya huduma za jumla. 

“Katika ukaguzi wa mwaka husika, Balozi zililipa Sh87.46 milioni kwa ajili ya kukodi magari,” imeeleza ripoti hiyo ambayo imeendelea kujadiliwa na wanawanchi katika maeneo mbalimbali nchini hususan kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari.

Hata hivyo, amebainisha kuwa menejimenti za balozi husika zimekuwa zikifanya ufuatiliaji wa karibu na wizara lakini hakuna dalili za kumaliza tatizo hilo ambalo linakiuka taratibu zilizowekwa. 

“Menejimenti za Balozi husika zimekuwa zikifanya ufuatiliaji wa karibu na Wizara mama kupitia barua yenye kumbukumbu Na. CJB111/162/02/16 ya tarehe 8 Novemba, 2017 na CKCA.41/65/01/III ya tarehe 15 Januari 2019, mtawalia, lakini hakuna kilichofanywa na wizara ili kumaliza tatizo hili,” inasomeka sehemu ya ripoti hiyo. 


Zinazohusiana:


CAG  ameishauri menejimenti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuachana na ongezeko la gharama za kukodi magari kwenye balozi kwa kuhakikisha inanunua magari yake.

Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro unaongozwa na Balozi Sylvester Mabumba huku Ubalozi wa Brazil ukiongozwa na Dk Emmanuel Nchimbi ambapo nchi hizo zimekuwa na ushirikiano wa muda mrefu hasa katika nyanja za mawasiliano na biashara ikiwemo mazao ya biashara.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.