Kisa corona, Twitter yafuta akaunti zaidi ya 170,000 za China

June 12, 2020 11:41 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Akaunti  zinazodaiwa zinauhusina na Serikali ya China.
  • Zimekuwa zikitumika kupotosha kuhusu Corona na masuala ya demokrasia.
  • Twitter yasema zilikuwa na wafuasi wachache na zinatumia lugha ya Kichina. 

Mtandao wa Twitter umetangaza kufuta akaunti zaidi ya 170,000 zenye mahusiano na Serikali ya China ikidai zimekuwa zikitoa habari mbalimbali za kupotosha ikiwemo ugonjwa wa virusi vya Corona. 

Twitter imesema katika taarifa yake iliyotolewa Juni 12, 2020 kuwa akaunti hizo pia zimekuwa zikisambaza propaganda zinazokipendelea Chama cha Ukomonisti cha China na kupinga maandamano ya raia wa Hong Kong.

Kufutwa kwa ukaunti hizo ambazo zilikuwa zinatumia zaidi lugha ya Kichina kunahusishwa na kukiuka sera za mtandao huo kwa sababu baadhi ya maudhui yake yalikuwa na viashiria vya uchochezi, ubaguzi na upotoshaji hasa ugonjwa wa COVID-19. 

Mtandao huo ulizuiwa kufanya kazi China, lakini watu wengi nchini humo wanautumia kwa mfumo wa maalum wa VPN. 


Zinazohusiana:


Kati ya akaunti zilizofutwa, 23,750 zilikuwa halali huku 150,000 zilibainika kuwa zilikuwa zinatumika kuzipa nguvu meseji ambavyo zilikuwa zinawekwa na akaunti hizo mtandaoni. 

Twitter imesema makundi hayo mawili ya akaunti yalikuwa na wafuasi wachache na muingiliano mdogo  wa watu mtandaoni. 

Kampuni hiyo ya Marekani imekuwa ikikosolewa vikali siku za hivi karibuni kutokana na sera yake ya kukaza uzi kudhibiti upotoshaji huku baadhi wakisema sera zake zinaweza kuminya uhuru wa kutoa maoni kuliko inavyodhaniwa. 

Huenda hatua hiyo ikasaidia katika mapambano ya COVID-19 ikizingatiwa kuwa baadhi ya watu hutumia janga hilo kupotosha umma. 

 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.