Kisa corona, Twitter yafuta akaunti zaidi ya 170,000 za China

June 12, 2020 11:41 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Akaunti  zinazodaiwa zinauhusina na Serikali ya China.
  • Zimekuwa zikitumika kupotosha kuhusu Corona na masuala ya demokrasia.
  • Twitter yasema zilikuwa na wafuasi wachache na zinatumia lugha ya Kichina. 

Mtandao wa Twitter umetangaza kufuta akaunti zaidi ya 170,000 zenye mahusiano na Serikali ya China ikidai zimekuwa zikitoa habari mbalimbali za kupotosha ikiwemo ugonjwa wa virusi vya Corona. 

Twitter imesema katika taarifa yake iliyotolewa Juni 12, 2020 kuwa akaunti hizo pia zimekuwa zikisambaza propaganda zinazokipendelea Chama cha Ukomonisti cha China na kupinga maandamano ya raia wa Hong Kong.

Kufutwa kwa ukaunti hizo ambazo zilikuwa zinatumia zaidi lugha ya Kichina kunahusishwa na kukiuka sera za mtandao huo kwa sababu baadhi ya maudhui yake yalikuwa na viashiria vya uchochezi, ubaguzi na upotoshaji hasa ugonjwa wa COVID-19. 

Mtandao huo ulizuiwa kufanya kazi China, lakini watu wengi nchini humo wanautumia kwa mfumo wa maalum wa VPN. 


Zinazohusiana:


Kati ya akaunti zilizofutwa, 23,750 zilikuwa halali huku 150,000 zilibainika kuwa zilikuwa zinatumika kuzipa nguvu meseji ambavyo zilikuwa zinawekwa na akaunti hizo mtandaoni. 

Twitter imesema makundi hayo mawili ya akaunti yalikuwa na wafuasi wachache na muingiliano mdogo  wa watu mtandaoni. 

Kampuni hiyo ya Marekani imekuwa ikikosolewa vikali siku za hivi karibuni kutokana na sera yake ya kukaza uzi kudhibiti upotoshaji huku baadhi wakisema sera zake zinaweza kuminya uhuru wa kutoa maoni kuliko inavyodhaniwa. 

Huenda hatua hiyo ikasaidia katika mapambano ya COVID-19 ikizingatiwa kuwa baadhi ya watu hutumia janga hilo kupotosha umma. 

 

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...