Kampuni tatu zilizopoteza soko la hisa Dar

August 19, 2019 1:48 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni Acacia, EABL na JHL ambazo thamani ya hisa zake zimeshuka kwa viwango tofauti. 
  • kampuni ya Jubilee Holdings Limited (JHL) ndiyo iliyofanya vibaya zaidi baada ya thamani ya hisa zake kushuka kwa asilimia 5.49.
  • Kampuni ya uwekezaji ya NICO yaongoza kwa kuuza kiwango kikubwa cha hisa. 

Dar es Salaam. Wawekezaji wa kampuni tatu katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) ikiwemo Acacia leo wamepoteza baada ya thamani ya hisa za kampuni hizo kushuka kwa viwango tofauti ikilinganishwa na ilivyokua ijumaa ya Agosti 16, 2019.

Ripoti ya soko ya siku ya DSE ya Agosti 19 inaonyesha kuwa hadi soko linafungwa jioni ya leo kampuni ya Jubilee Holdings Limited (JHL) ndiyo iliyofanya vibaya zaidi baada ya thamani ya hisa zake kushuka kwa asilimia 5.49 ambapo wawekezaji wake wamepoteza Sh450 kwa kila hisa moja. 

Ripoti hiyo inaonyesha kuwa hadi soko linafungwa thamani ya hisa moja ya JHL ilikuwa ni Sh7,750 kutoka Sh8,200 iliyorekodiwa ijumaa.

Kampuni nyingine ambayo thamani ya hisa zake zimeshuka ni pamoja na Acacia ambayo imeporomoka kwa asilimia 0.74 ambapo hadi soko linafungwa hisa moja ya kampuni hiyo ilikuwa inauzwa Sh6,750 ukilinganisha na Sh6,800 ya ijumaa.  

Pia thamani za hisa za kampuni ya bia ya Afrika Mashariki (EABL) zimeshuka kiduchu kwa asilimia 0.67 ambapo wawekezaji wake wamepoteza Sh30 kwa kila hisa. 


Zinazohusiana: 


Wakati kampuni hizo tatu zikipoteza, hakuna hata kampuni moja ambayo thamani ya hisa zake imepanda katika soko hilo huku nyingi zikibaki katika viwango vilivyokuwepo Ijumaa iliyopita  zikiwemo Vodacom, na benki ya CRDB na DCB. 

Hata hivyo, kampuni ya uwekezaji ya NICO ndiyo iliyofanya vizuri zaidi leo baada ya kuongoza kwa kuuza kiwango kikubwa cha hisa. 

NICO imeuza hisa 17,200 sawa na asilimia 58.5 ya hisa zote zilizouzwa sokoni leo huku ikifuatiwa kwa mbali na benki CRDB ambayo imeuza hisa 12,000 na Soko la Hisa la Dar es Salaam hisa 133. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.