Instagram yazindua akaunti maalum ya kuuza bidhaa mtandaoni

May 14, 2019 1:29 pm · Daniel
Share
Tweet
Copy Link

Kuundwa kwa akaunti hiyo ni jitihada za Instagram katika kutanua wigo wa biashara ambapo awali ilikuwa ikitegemea zaidi matangazo kama sehemu ya kupata mapato. Picha|Mtandao. 


  • Akaunti hiyo inatumika kuwaleta pamoja wanunuzi na wauzaji wa bidhaa mbalimbali.
  • Ni jitihada nyingine ya mtandao huo kuwapa watumiaji vitu wanavyotaka. 

Mtandao wa kijamii wa Instagram umezindua akaunti mpya ya @shop maalum ili kuwahudumia watumiaji wake wanaopendelea kufanya manunuzi mtandaoni. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mtandao huo, @shop imetengenezwa na kuingizwa sokoni kwa ajili ya kuwaleta pamoja na kuwaunganisha wauzaji na wanunuzi wa bidhaa mtandaoni. 

Akaunti hiyo inaendesha manunuzi kwa kutumia picha za bidhaa mbalimbali zinazochapishwa katika kurasa zake ambapo kwa kuanzia imeweka bidhaa za urembo, mitindo, mapambo ya nyumbani na nguo. 

Haitatumika tu kama jukwaa la kutangaza bidhaa, bali itawawezesha watumiaji wake kufanya manunuzi moja kwa moja pasipo kutumia mifumo mingine mbali na mtandao huo. 

Akaunti hiyo imeanza kujipatia umaarufu mkubwa mara tu baada ya kuzinduliwa ambapo mpaka mchana wa leo (Mei 14, 2019) ilikuwa na wafuasi zaidi ya 50,000 huku ikiwa na machapisho 15 tu yanayonyesha bidhaa mbalimbali.


Zinazohusiana: 


Kuundwa kwa akaunti hiyo ni jitihada za Instagram katika kutanua wigo wa biashara ambapo awali ilikuwa ikitegemea zaidi matangazo kama sehemu ya kupata mapato lakini sasa itakuwa sehemu muhimu kwa watu kupata bidhaa mbalimbali kutoka kona mbalimbali za dunia.  

Biashara ya mtandaoni huusisha uuzaji na ununuzi wa bidhaa kwa kutumia mifumo ya kidijitali ambapo watu hawalazimiki kwenda dukani au sokoni lakini kwa kutumia simu au kompyuta anaweza kupata bidhaa au huduma popote alipo. 

Vichocheo vikubwa vya mfumo wa biashara ya mtandaoni ni maendeleo ya teknolojia hususani ueneaji wa mtandao wa intaneti katika maeneo mbalimbali na uwepo wa makampuni ya simu za mkononi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
26 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
26 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV