Hapana: Siyo lazima kupima Uviko-19 kabla ya kupata chanjo

October 12, 2022 5:36 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Kila mtu ana haki ya kupata chanjo.
  • Sio lazima mtu anayetaka kupata chanjo apime Corona.

Dar es Salaam. Wakati dunia ikiendelea na mapambano juu ya ugonjwa wa Uviko-19 na kuhamasisha chanjo, kumeibuka taarifa za uzushi kuwa ili uweze kupata chanjo ya ugonjwa huo ni lazima upime na uwe tayari umeshaambukizwa ugonjwa huo.

Taarifa hizo zinazosambaa kwenye jamii na mitandao ya kijamii sio za kweli.

Shirika la Afya Duniani (WHO)  inasema kila mtu ana haki ya kupata chanjo, kwa wakati wowote ili kuzuia kusambaa zaidi kwa ugonjwa huo na hatari za vifo.

“Siyo lazima mtu anayetaka kupata chanjo awe amewahi kupata ugonjwa huo au apime kwanza ndipo apewe chanjo,” anasema  Dk Phionah Atuhebwe, Afisa Chanjo kutoka WHO.

Hata hivyo, Afisa huyo amesema ikiwa vipimo vitaonyesha  umeambukizwa  Uviko-19 unatakiwa kujitenga na kupata matibabu kabla ya kupata chanjo ya ugonjwa huo.


Zinazohusiana


Nani haruhusiwi kupata chanjo?

Sambamba na hayo WHO imeainisha mazingira ambayo mtu hataruhusiwa kupata chanjo.

Hutaruhusiwa kupata chanjo ikiwa una mzio na moja ya viambata vilivyopo kwenye chanjo za Uviko-19 ili kuzuia madhara zaidi ya kiafya yanayoweza kutokea.

Ikiwa joto lako la mwili limezidi nyuzijoto 38 hairisha mpango wa kupata chanjo mpaka joto litakaposhuka.

Hutaruhusiwa kupata chanjo ikiwa umethibitisha kupata Uviko 19 siku za karibuni. Wataalamu wanashauri mgonjwa asubiri hadi muda  wa kujitenga ukamilike na dalili za ugonjwa huo ziwe zimeisha.

Kwa wanaotumia dawa za kupunguza damu  wanashauriwa kumtaarifu mtoa chanjo kabla ya kupata chanjo yoyote ya Uviko-19.

WHO inasema Japo ni salama  kupata chanjo ukiwa kwenye hali hiyo lakini kutoa taarifa mapema ni muhimu kwani kutamsaidia mtoa huduma kukupa ushauri na kutoa huduma za ziada zitakapohitajika.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW