Google Maps yawakumbuka tena watumiaji wa simu za Iphone

October 21, 2019 12:55 pm · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Inawawezesha kujua hali ya barabara wakati wowote kwa kuwajulisha kama kuna ajali imetokea, barabara inajengwa au imefungwa.
  • Mabadiliko haya yanasaidia watumiaji wa barabara kupata taarifa mapema kabla hawajapoteza mafuta na muda mwingi barabarani.
  • Huduma hiyo tayari inatumika katika simu za Android. 

Watumiaji wa simu za Iphone, sasa wana kila sababu ya kutabasamu kwa sababu kampuni ya Google inazidi kuwasogelea kila siku kwa huduma mbalimbali za teknolojia.

Safari imefungua mlango kwa watumiaji wa simu hizo kutumia bidhaa yake ya “Google Maps” iliyoboreshwa zaidi ambayo inawawezesha kujua hali ya barabara wakati wowote kwa kuwajulisha kama kuna ajali imetokea, barabara inajengwa au inafanyiwa ukarabati.

Pia inawasaidia watumiaji wa simu hizo zinazotumia programu endeshi ya iOS kujua kama barabara wanayotaka kutumia kama imefungwa na haitumiki kwa wakati husika. 

Huduma hiyo ambayo tayari ilianza kutumika kwa watumiaji wa simu za Android, inalenga kumrahisishia maisha mtumiaji wa barabara na kumpunguzia muda wa kukaa barabarani muda mrefu na gharama za mafuta.  


Zinazohusiana: 


Ili kupata taarifa ya barabara unayotaka kutumia, unapaswa kwenda Google Maps, kisha bonyeza kitufye chenye alama ya kuweka tukio jipya chini ya alama inayoonesha mwelekeo (compass direction) kisha ataweka taarifa yako ya unakokwenda.

Baada ya kuweka taarifa zako, utaletea taarifa zote za barabara husika ikiwemo hali ya foleni  kama ambavyo zimekuwa zikitolewa awali na picha halisi ya kizuizi cha barabarani kama ni ajali, ujenzi au barabara imefungwa.

Kwa sasa, mtumiaji wa Google Maps, anaweza kujua mwendo anaotakiwa kutembea akiwa barabarani kulingana na foleni na hali ya foleni katika barabara mbalimbali z aeneo lake. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.