Google Maps yawakumbuka tena watumiaji wa simu za Iphone

October 21, 2019 12:55 pm · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Inawawezesha kujua hali ya barabara wakati wowote kwa kuwajulisha kama kuna ajali imetokea, barabara inajengwa au imefungwa.
  • Mabadiliko haya yanasaidia watumiaji wa barabara kupata taarifa mapema kabla hawajapoteza mafuta na muda mwingi barabarani.
  • Huduma hiyo tayari inatumika katika simu za Android. 

Watumiaji wa simu za Iphone, sasa wana kila sababu ya kutabasamu kwa sababu kampuni ya Google inazidi kuwasogelea kila siku kwa huduma mbalimbali za teknolojia.

Safari imefungua mlango kwa watumiaji wa simu hizo kutumia bidhaa yake ya “Google Maps” iliyoboreshwa zaidi ambayo inawawezesha kujua hali ya barabara wakati wowote kwa kuwajulisha kama kuna ajali imetokea, barabara inajengwa au inafanyiwa ukarabati.

Pia inawasaidia watumiaji wa simu hizo zinazotumia programu endeshi ya iOS kujua kama barabara wanayotaka kutumia kama imefungwa na haitumiki kwa wakati husika. 

Huduma hiyo ambayo tayari ilianza kutumika kwa watumiaji wa simu za Android, inalenga kumrahisishia maisha mtumiaji wa barabara na kumpunguzia muda wa kukaa barabarani muda mrefu na gharama za mafuta.  


Zinazohusiana: 


Ili kupata taarifa ya barabara unayotaka kutumia, unapaswa kwenda Google Maps, kisha bonyeza kitufye chenye alama ya kuweka tukio jipya chini ya alama inayoonesha mwelekeo (compass direction) kisha ataweka taarifa yako ya unakokwenda.

Baada ya kuweka taarifa zako, utaletea taarifa zote za barabara husika ikiwemo hali ya foleni  kama ambavyo zimekuwa zikitolewa awali na picha halisi ya kizuizi cha barabarani kama ni ajali, ujenzi au barabara imefungwa.

Kwa sasa, mtumiaji wa Google Maps, anaweza kujua mwendo anaotakiwa kutembea akiwa barabarani kulingana na foleni na hali ya foleni katika barabara mbalimbali z aeneo lake. 

/
No matches found for this filter
10 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
10 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
10 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa kiwango cha biashara kati ya Tanzania na Sin

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa kiwango cha biashara kati ya Tanzania na Sin

Nukta TV

Mizinga ya heshima, Rais Samia akimpokea Rais wa Singapore, Ikulu Dar es Salaam

Mizinga ya heshima, Rais Samia akimpokea Rais wa Singapore, Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Mikakati ya Serikali kuhakikisha walimu wa VETA wanapata ajira na mikopo

Mikakati ya Serikali kuhakikisha walimu wa VETA wanapata ajira na mikopo

Nukta TV