Dola, Euro na Pauni zaendelea kuimarika dhidi ya Shilingi Mei 28, 2026
- Dola ya Marekani (USD) kupitia Benki ya CRDB imenunuliwa kwa Sh2,585 na kuuzwa kwa Sh2,665.
Sarafu kuu za kimataifa zimeendelea kuonyesha nguvu dhidi ya Shilingi ya Tanzania leo Mei 28, 2026 ukilinganisha na Hali ilivyo kuwa katika wiki zilizopita.
Viwango vya ubadilishaji fedha kutoka Benki za CRDB na NMB vinaonesha kupanda kwa sarafu hizo ikiwemo Dola ya Marekani, Euro pamoja na Pauni ya Uingereza.
Katika viwango vya leo, Dola ya Marekani (USD) kupitia Benki ya CRDB imenunuliwa kwa Sh2,585 na kuuzwa kwa Sh2,665, huku kupitia Benki ya NMB ikinumuliwa kwa Sh2,583 na kuuzwa kwa Sh2,663.
Mwenendo wa leo unaonyesha kuwa mahitaji ya sarafu za kigeni yanaendelea kuongezeka katika soko la ndani, hali inayoweza kuathiri gharama za biashara za kimataifa, usafirishaji wa bidhaa kutoka nje pamoja na huduma zinazotumia fedha za kigeni.