Dk Mpango awaonya wanaotumia fedha za umma vibaya

November 26, 2020 6:18 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Amesema Serikali itawachukulia hatua kali za kisheria.
  • Ayataka mabaraza ya madiwani kusimamia vizuri fedha miradi ya maendeleo. 

Dar es Salaam. Siku chache baada ya Dk Philip Mpango kuchaguliwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango, ameonya kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua kali kwa watumishi wa umma watakaojihusisha na vitendo vya ufisadi, ubadhirifu wa fedha za umma utakaoisababishia Serikali hasara.

Dk Mpango ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Buhigwe mkoani Kigoma, ni miongoni mwa waziri wa mwanzo kuchaguliwa na Rais John Magufuli kuingia katika Baraza la Mawaziri katika Serikali ya awamu ya sita. 

Mpaka sasa baraza hilo lina mawaziri wawili akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof Palamagamba Kabudi. 

Waziri Mpango aliyekua akizungumza Novemba 25, 2020 na wananchi wa kata ya Mnanila mkoani Kigoma amesema watumishi wa umma wanapaswa kufanya kazi kwa bidii na uadilifu ili kuwatumikia vema wananchi. 

“Hao mafisadi na wabadhirifu wa fedha za umma nawaonea huruma kwa sababu kisu nimepewa mwenyewe na Waziri wa Fedha hana mipaka, popote ilipo fedha na mali ya umma, akawapo mwizi, mbadhirifu, huyo ni halali yangu” amesema Dk Mpango.


Soma zaidi: 


Aidha, ameyaagiza mabaraza ya madiwani kote nchini, kuhakikisha kuwa fedha za miradi zinazotumwa na Serikali katika maeneo yao zinasimamiwa vizuri ili kuleta tija na maendeleo ya jamii.

“Kwa hiyo lazima tufanye kazi ya kukusanya mapato na kutumia fedha vizuri ili watumishi hawa wanaohangaika kila siku na walau wapate kamshahara ambako kanasaidia zaidi” amesisitiza waziri huyo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
6 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
6 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Fahamu kuhusu 'BIPOLAR' | Ugonjwa hatari unaoathiri na kubadili hisia

Fahamu kuhusu 'BIPOLAR' | Ugonjwa hatari unaoathiri na kubadili hisia

Nukta TV

Je, ’BIPOLAR’ ina uhusiano na kupenda kufanya tendo la ndoa zaidi?

Je, ’BIPOLAR’ ina uhusiano na kupenda kufanya tendo la ndoa zaidi?

Nukta TV

Hii ndio sababu uhusiano wa kimapenzi ni marufuku makazini

Hii ndio sababu uhusiano wa kimapenzi ni marufuku makazini

Nukta TV