Dar es salaam yaongoza maambukizi ya Uviko-19 Julai

August 27, 2022 10:21 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Yachukua zaidi ya theluthi mbili ya maambukizi.
  • Wananchi wahimizwa kupata Chanjo. 

Dar es Salaam. Mkoa wa Dar es salaam umeongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya maambukizi mapya ya ugonjwa wa Uviko-19 nchini Tanzania mwezi uliopita wa Julai.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Afya kuhusu mwenendo wa ugonjwa wa Uviko-19 iliyotolewa hivi karibuni, imebainisha kuwa kati ya wagonjwa 543 walioripotiwa Julai 2 hadi 29, wagonjwa 366 wametoka Mkoa wa Dar es salaam.

Hiyo ni sawa kusema takriban wagonjwa 7 kati ya 10 walitoka katika mkoa huo.

Kati ya wagonjwa hao 543,  watu 10 walilazwa huku wote wakiwa hawajachanja.

Hadi kufikia Julai 29 mwaka huu,  jumla ya watu 38,201 wamepata maambukizi ya Uviko-19 nchini Tanzania huku 801 wakipoteza maisha.

Wananchi wameaswa kuendelea kuchukua tafadhali kwa kupata chanjo ya Uviko-19, kuvaa barakoa, kuosha mikono kwa sabuni na maji tiririka. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
NISHATI

NISHATI

Nukta TV

Utani wa Rais Samia kwa wachimba madini wa Katoro

Utani wa Rais Samia kwa wachimba madini wa Katoro

Nukta TV

Rais Samia: Misaada imepungua, tukaze buti

Rais Samia: Misaada imepungua, tukaze buti

Nukta TV