Dar es salaam yaongoza maambukizi ya Uviko-19 Julai
- Yachukua zaidi ya theluthi mbili ya maambukizi.
- Wananchi wahimizwa kupata Chanjo.Â
Dar es Salaam. Mkoa wa Dar es salaam umeongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya maambukizi mapya ya ugonjwa wa Uviko-19 nchini Tanzania mwezi uliopita wa Julai.
Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Afya kuhusu mwenendo wa ugonjwa wa Uviko-19 iliyotolewa hivi karibuni, imebainisha kuwa kati ya wagonjwa 543 walioripotiwa Julai 2 hadi 29, wagonjwa 366 wametoka Mkoa wa Dar es salaam.
Hiyo ni sawa kusema takriban wagonjwa 7 kati ya 10 walitoka katika mkoa huo.
Kati ya wagonjwa hao 543, Â watu 10 walilazwa huku wote wakiwa hawajachanja.
Hadi kufikia Julai 29 mwaka huu, Â jumla ya watu 38,201 wamepata maambukizi ya Uviko-19 nchini Tanzania huku 801 wakipoteza maisha.
Wananchi wameaswa kuendelea kuchukua tafadhali kwa kupata chanjo ya Uviko-19, kuvaa barakoa, kuosha mikono kwa sabuni na maji tiririka.Â
