Daniel Sillo achaguliwa Naibu Spika  Bunge la 13 Tanzania

November 13, 2025 3:22 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Apata asilimia 100 za kura za ndio zilizopigwa na wabunge 371 waliohudhuria kikao.

Dar es Salaam. Wabunge wamechagua Daniel Sillo kuwa Naibu Spika wa Bunge baada ya kumpa kura zote za ndio sawa na asilimia 100 ya kura zilizopigwa na wabunge 371 waliohudhuria kikao

Uchaguzi wa Sillo umefanyika kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, inayobainisha kwamba Naibu Spika atachaguliwa na wabunge kutoka wabunge waliochaguliwa, na kupigiwa kura baada ya kupendekezwa.

Sillo ni Mbunge wa jimbo la Babati Vijijini ambaye kwa uzoefu pia, amewahi kushika nafasi ya Uenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti.

Wakati Sillo akichaguliwa, Bunge linaendelea kujiandaa kusikiliza hotuba ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye anatarajia kulihutubia Bunge hapo kesho Novemba 14, 2025 kama ilivyo kwa mujibu wa sheria. 

Shughuli za Bunge katika kikao cha leo zilikuwa ni kuchagua Naibu Spika wa Bunge pamoja na kumpitisha Waziri Mkuu wa Tanzania ambapo Rais Samia amempendekeza aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba na wabunge kumptitisha kwa kura 369 za ndio akirithi nafasi hiyo iliyokuwa ikishikiliwa na Kassim Majaliwa. 

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW