Rais Samia ateua sita, kuwa wabunge wa Tanzania

November 10, 2025 5:27 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Miongoni mwa walioteuliwa ni pamoja na Dorothy Gwajima na Balozi Mahmoud Thabit Kombo .

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa wabunge sita wa Bunge la Tanzania.

Taarifa iliyotolewa leo Novemba 10, 205 na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dk Moses Kusiluka imeeleza kuwa uteuzi huo ni kwa mujibu wa  Ibara ya 66(1)(e) ya Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977.

Miongoni mwa walioteuliwa ni pamoja na Dk Dorothy Gwajima, Balozi Mahmoud Thabit Kombo na Balozi Dk Bashiru Ally Kakurwa.

Vile vile, amewateua  Abdullah Ali Mwinyi, Balozi Khamis Mussa Omarna na Dk Rhimo Simeon Nyansaho.

Uteuzi huu unakuja siku saba  baada ya Rais Samia kuapishwa kuwa Rais wa Tanzania baada ya kushinda katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 29, 2025.

Kwa mujibu wa Matokeo rasmi yaliyotangazwa Novemba 1, 2025 na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Ramadhan Kairima, Samia, alitangazwa mshindi baada ya kupata kura milioni 31.91 sawa na asilimia 97.66 ya kura halali milioni 32.67 zilizopigwa.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV