Chanjo zilizookoa maisha ya watu kabla ya Uviko-19

August 31, 2021 8:44 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na chanjo ya pepopunda na polio.
  • Chanjo hizo zimeokoa maisha ya wengi wakiwemo Watanzania.

Dar es Salaam. Mjadala wa chanjo ni kati ya mijadala iliyoshika kasi mwaka 2021. Kutokana na ukosefu wa taarifa sahihi miongoni mwa watu, kila mtu anaibuka na nadharia zake kuhusu chanjo ya Uviko-19 inayotolewa kwenye nchi mbalimbali duniani.

Wapo walioikubali na hadi sasa wamepata dozi zao za chanjo lakini wapo ambao kukosa taarifa sahihi kunawafanya waendelee kuhoji uthabiti wa chanjo hiyo.

Hata hivyo, ni muhimu kujua kuwa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Uviko-19 siyo chanjo ya kwanza kutolewa duniani. Zipo chanjo dhidi ya magonjwa mbalimbali ambazo zinatolewa kwa watu duniani ili kuwakinga na magonjwa hatarishi.

Mathalan, chanjo dhidi ya magonjwa kama polio, pepopunda, surua na mafua, ni chanjo ambazo zimeokoa maisha ya watu wengi wakiwemo watoto walio na umri chini ya miaka mitano.

Kufahamu zaidi kuhusu chanjo hizo, tazama video hii fupi.

                       

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW