BoT yatoa tahadhari matumizi ya fedha za kimtandao Tanzania

November 12, 2019 9:56 am · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Yasema imegundua matukio mbalimbali yanayohusisha uhamishaji wa biashara na matumizi ya fedha za kimtandao nchini.
  • Yabainisha kuwa fedha hizo ni kinyume cha kanuni zilizopo za fedha za kigeni na kunaweza kusababisha hasara kwa anayehusika.

Dar es Salaam. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imewatahadharisha Watanzania kutojihusisha na fedha za kimtandao na kwa kufanya hivyo ni kinyume cha kanuni zilizopo za fedha za kigeni na kunaweza kusababisha hasara kwa anayehusika. 

BoT katika taarifa yake iliyotolewa leo (Novemba 12, 2019) imesema  imeshuhudia kuwepo kwa wananchi wanaotumia fedha za kimtandao (cryptocurrencies) katika kufanya malipo hapa nchini. 

Imesema inatambua kuwa kuna matukio ya kuhamasisha biashara ya fedha hizo za kimtandao hapa nchini ili zionekane kama ni fedha halali kwa ajili ya kufanya malipo. 

“Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuutahadharisha umma kwamba uuzaji, uhamasishaji wa biashara hiyo na matumizi ya fedha za kimtandao ni kinyume cha kanuni za udhibiti wa fedha za kigeni,” inasomeka na sehemu ya taarifa hiyo.


Zinazohusiana:


BoT, kama taasisi pekee hapa nchini yenye mamlaka ya kuchapisha noti na kutengeneza sarafu na kuamua fedha halali kwa ajili ya matumizi hapa nchini inautarifu umma kwamba Shilingi ya Tanzania ndiyo fedha halali kwa ajili ya kufanya malipo hapa Tanzania. 

“Fedha zingine za kigeni zinauzwa na taasisi zilizosajiliwa hapa nchini kwa mujibu wa taratibu zilizopo za kubadilisha fedha za kigeni. Fedha hizo zinazonunuliwa zinarudishwa kwenye nchi husika kwa mujibu taratibu zilizopo,” inaeleza taarifa hiyo.

“cryptocurrencies” ni sehemu ya “blockchain”; teknolojia ya mfumo unaomruhusu mtu kutuma au kuhifadhi vitu vyake zikiwemo nyaraka na pesa kwa njia ya mtandao bila kumuhusisha mtu mwingine (third party) au kupitia kwa sehemu nyingine ambayo haihusiki.

Katika teknolojia hiyo ya blockchain ni vigumu mtu yeyote aliyepo kwenye mfumo kufanya uchakachuaji katika masuala ya miamala bila wahusika wote kuthibitisha.

Kwa Tanzania, mfumo huo wa malipo bado haujaanza kutumika rasmi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV