Jinsi ya kupika supu ya samaki

February 20, 2025 6:19 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Supu hii sio tu ni tamu pia ina virutubisho muhimu kama protini,mafuta na vitamini A,na B.
  • Unaweza kuandaa kwa ajili ya familia au biashara.

Supu ya samaki ni chakula chepesi lakini chenye nguvu, likichosheheni ladha tamu inayoweza kutumiwa na watu wa rika zote ikiwemo watoto, wanawake waliotoka kujifungua au wazee.

Pamoja na kutumiwa sana na makundi hayo, mlo huo pia una wingi wa virutubisho muhimu kama Protini , mafuta, madini ya chuma, vitamini A, vitamini B, kalsiamu, zinki, magnesiamu, fosforasi na  seleniumu kwa mujibu wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) 

Faida hizo za kiafya hupoatikana kutokana na matumizi ya samaki na mboga mboga ikiwemo karoti, pilipili hoho zinazotumika kunogesha zaidi pishi hilo.

Supu ya samaki hutumiwa zaidi wakati wa kifungua kinywa asubuhi huku wengine wakiitumia jioni kama mlo wa usiku ikisindikizwa na vitafunwa kama chapati, maandazi au mikate.

Ikiwa unapenda supu ya samaki na haujui jinsi ya kuiandaa usiwaze, leo jiko point imekuletea maandalizi rahisi ya mlo huo kwa kutumia mahitaji machache yanayopatikana kwa urahisi nyumbani.

Namna ya kuandaa hatua kwa hatua

Hatua ya kwanza chukua samaki na uwasafishe vizuri hakikisha umewaosha na kuwatoa magamba kama wanayo.

Baada ya hapo chukua sufuria kubwa kishaa weka samaki muache akauke yale maji ya shombo kidogo ila kuwa makini asishikie kwenye sufuria.

Hatua inayofuata ni kuongeza  maji katika sufuria hiyo hiyo ikifuatiwa na mafuta ya kula vijiko viwili, itapendeza zaidi kama ukitumia mafuta ya zaituni, alizeti au karanga maana ndio mazuri kwa afya kisha acha ichemke.

Maji yakianza kuchemka, punguza moto na uache samaki waive kwa dakika 15 mpaka 20 ikifuatiwa na kitunguu, chumvi kiasi na karoti na uafunike viive.

Baada ya dakika tano ongeza limao na hoho ukipenda unaweza kuweka pilipili, mbogamboga kidogo kama kabichi, brokoli ama mchicha ili kuongeza ladha zaidi.

Ukimaliza hatua hizo zote supu yako ya samaki itakuwa tayari kwa kuliwa na unaweza kula kwa chapati, maandazi au ukaitumia yenyewe na mambo yakawa murua.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
12 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
12 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV