Namna rahisi ya kupika samaki makange, wali maua nyumbani

July 18, 2022 6:10 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link

Kuna wanaodhani samaki makange wa kupika nyumbani sio mtamu kama wale wanaopatikana hotelini, migahawani au kwa mama ntilie.

Leo tumekuletea maujanja ya kupika samaki makange nyumbani na ladha yake ifanane na ladha ya migahawani au hotelini.

Samaki makange anaweza akaliwa na ugali, wali, tambi au chipsi ila leo tutaandaa samaki makange atakayeliwa na wali maua.

Maandalizi

Hatua ya kwanza ni kuosha samaki na kumuandaa kwa ajili ya kumkaanga. Hapa unaweka tangawizi, kitunguu swaumu, ndimu kiasi na masala.

Kisha funika samaki wako na umuache  kwa dakika 10 mpaka 20 ili viungo viingie ndani ya samaki vizuri.

Wakati unasubiri viungo vienee kwenye samaki unaweza kupika wali, kwa kuanza na kuchambua mchele  kuosha hoho na  karoti kisha ukate kwa saizi ya boksi ili kuleta muonekano mzuri. Menya  njegere na uzioshe.

Washa jiko na uchemshe maji ya moto utakayoyatumia kupika wali, yakichemka weka sufuria nyingine jikoni, ongeza mafuta kiasi utakayoyatumia kukaanga viungo vya kupika wali.

Mafuta yakipata moto weka vitunguu na ukaange mpaka viwe vya rangi ya kahawia kisha ongeza karoti na njegere na ukaange kwa muda. Malizia kwa kuongeza maji  kiasi yatakayotosha kuivisha wali.

Yakichemka ongeza chumvi kiasi, na uongeze mchele uliochambua na kuosha vizuri mwanzoni. Funika uache uive wa moto mdogo.

Wakati wali unaiva tuandae makange yetu sasa.

Weka mafuta jikoni yakichemka mkaange samaki wako kwa moto mdogo mpaka awe na rangi ya kahawia, wakati ukisubiri samaki aive unaweza kuosha nyanya, kitunguu, karoti na hoho kwa ajili ya kuunga samaki akiiva.

Saga nyanya na karoti kwenye brenda au unaweza kusaga kwenye kisagio cha mkono, hoho na karoti nyingine ukate kwa saizi ya urefu ili vilete muonekano mzuri wa makange yako.

Samaki akiiva vizuri, weka sufuria nyingine jikoni na ukaange vitunguu, weka nyanya na karoti uliyosaga na uache vichemke.

Weka samaki wako kisha ufunike kwa dakika tano baada ya hapo ongeza chumvi, ndimu na viungo vingine vilivyobakia. Hakikisha mchuzi unakuwa mzito na uongeze pilipili kama unapendelea.

Weka tui la nazi au nazi ya pakti ili kuongeza ladha zaidi. Samaki makange sasa ipo tayari kuliwa na wali wa maua.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV