Namna ya kupika samaki bila mafuta

June 9, 2022 10:23 am · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Unaweza kufanya hivyo ikiwa una nazi, nyanya chungu na bamia.

Mara nyingi wapishi wamezoea kutumia mafuta kama moja ya kiungo kinacholeta ladha kwenye chakula. Lakini leo naomba tujaribu kupika mboga aina ya samaki bila kutumia mafuta yaani mboga na nazi pekee.

Jikoni kwetu leo mboga yetu leo ni samaki ambaye tutaenda kumuandaa kwa ajili ya chakula cha jioni au mchana.

Mahitaji ni samaki wabichi au wakavu, nyanya maji, kitunguu maji, karoti, nyanya chungu, bamia, ndimu au limao, nazi kubwa moja na chumvi.

Baada ya kuandaa viungo hivi, kinachofuata ni kuchukua Samaki wakavu loweka kwenye maji ya moto hadi walainike kama ni samaki wabichi wachemshe au wakaange kwanza.

Wakati unaloweka au kuwachemsha hakikisha umewamiminia limao na tangawizi kisha waache ndani ya dakika 15. Baada ya hapo katakata kitunguu na nyanya kisha saga karoti.

Anza kupika pishi lako

Bila kuweka mafuta bandika sufuria jikoni kisha mimina hivyo viungo na samaki kwa pamoja ongeza maji kidogo acha vichemke kisha kamulia ndimu au limao.

Wakati hivyo viungo vikiwa jikoni vinachemka weka bamia, nyanya chungu na samaki kisha changanya. Mimina tui la pili la nazi lile jepesi kiasi kisha bila kufunika  acha viive.

Baada ya tui la pili kukauka weka tui la kwanza lile zito na mimina chumvi kiasi changanya acha mboga ichemke hadi iive. Baada ya hapo mboga itakuwa tayari kwa chakula unaweza kuitumia kwa ugali, wali au ndizi za kuchemsha.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV