Ashtakiwa kwa kujiteka ili apate mtaji Mwanza

April 24, 2024 2:52 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Alijiteka ili kujipatia mtaji wa Sh5 milioni kutoka kwa ndugu na marafiki zake wa karibu.
  • Jeshi la Polisi limetoa onyo kwa watu kuacha tabia iliyooneshwa na kijana huyo.

Mwanza. Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza linawashikilia watu saba katika matukio mawili tofauti akiwemo Zayoga John (28) mkazi wa mtaa wa Mkuyuni wilayani Nyamagana aliyejiteka ili kujipatia mtaji.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, April 24, 2024, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza DCP Wilbrod Mutafungwa amesema tukio hilo lilitokea April 9 mwaka huu ambapo watu wafanyabiashara wawili ambao ni George Mapunda (34) na Veronica Zayoga alipotoa taarifa juu ya kutoweka kwa mfanyabiashara mwenzao huku jitihada za kumtafuta zikigonga mwamba.

“Wakati upelelezi wa tukio hilo ukiendelea, April 11 tulifanikiwa kupata taarifa kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki kuwa Zayoga kwa muda tofauti amekuwa akiwapigia ndugu zake akiwajulisha kuwa ametekwa na watekaji alimtaka kutoa kiasi cha Sh10 milioni ili wamwachie,” amesema DCP Mutafungwa

Kwa mujibu wa DCP Mutafungwa, Zayoga aliwaeleza nduzu zake kuwa kati ya fedha hizo tayari amewapatia kiasi cha Sh5 milioni kutoka kwenye akaunti yake ya benki na kuwa hawatomwachiwa iwapo hatakamilisha kiasi hicho.


Soma zaidi:Bajeti ya Wizara ya Nishati Tanzania yapungua kwa Sh1.1 trilioni


DCP Mutafungwa amesema makachero wa Jeshi la Polisi waliendelea na ufuatiliaji wa kina kuhusu tukio hilo huku wakishirikiana na taasisi nyingine za Serikali kwa kufuatilia mienendo ya tukio hilo toka alipofika kituoni hapo April 3 mwaka huu akidai kufuatiliwa na watu wasiojulikana waliokuwa wanatumia gari aina Toyota ‘land cruiser’ rangi ya fedha (silver).

“Ilipofika Aprli 13 huko  Tunduma mkoani Songwe, Jeshi la Polisi lilifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo  akiendelea na shughuli zake na mwenye afya njema na baada ya mahojiano aliweka wazi kuwa aliamua kutoa taarifa za uongozo ili aweze kujipatia fedha za mtaji wa biashara yake ya kuuza mbao,”amesema DCP Mutafungwa

Hata hivyo Jeshi la Polisi linatoa onyo kwa watu kuacha tabia iliyoonyeshwa na kijana huyu kuwa halitawafumbia macho wote watakaohusika kupotosha umma na kijana tayari ameshafanyiwa uchunguzi wa kitabibu na atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka.

Watuhumiwa wengine waliokamatwa ni pamoja Iddy Hamis(30), Method Charles (44), Mikweba  Irangi (53) Freddy Nyakega(46) na Salumu Hussein( 32) wanaoshtakiwa  kuiba mabomba ya maji ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Mwauwasa).

Mwingine ni Kelvin Boneth  ambaye anatuhumiwa kuiba gari aina ya BMW.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Nukta TV

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Nukta TV

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Nukta TV