CAG awaweka matatani watumishi watatu Nkasi

June 4, 2020 6:41 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Wanadaiwa kula Sh27.6 milioni za makusanyo na kujikopesha bila ya kuziwasilisha benki.
  • CAG aipa Halmashauri hiyo hati ya mashaka kwa utata wa mapato. 
  • TAKUKURU yaagizwa kuwakamata na kuwachukulia hatua. 

Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Nkasi kuwakamata watumishi watatu wa halmashauri hiyo kwa kula Sh27.6 milioni za makusanyo na kujikopesha bila ya kuziwasilisha benki.

Wangabo ameipa TAKUKURU siku saba kuhakikisha watumishi hao wanarudisha fedha hizo na endapo watashindwa kufanya hivyo basi wafikishwe mahakamnami haraka iwezekanavyo.

“Nimeambiwa hizi fedha zinawahusu watumishi wa halmashauri watatu, mmoja anadaiwa Sh4 milioni, na wengine wawili Sh9 milioni (kila mmoja), imesemwa tu wachukuliwe hatua za kisheria, lakini haikutoa muda, hadi lini hawa watu wawe wamechukuliwa hatua hizo za kisheria?, 

“TAKUKURU mko hapa, kamata hawa watumishi watatu, shughulikeni nao haraka iwezekanavyo kuanzia leo,” amesema Wangabo jana katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi.

Hata hivyo, Mkuu huyo wa mkoa hawajawataja watumishi hao kwa majina na vyeo vyao. 

Kikao hicho kilikuwa kinajadili utekelezaji wa hoja za ukaguzi na mapendekezo ya Mdhibiti na Makaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2018/2019. 


Soma zaidi:


Amesema kwa mujibu wa  CAG kwa mwaka wa fedha 2018/2019, mapato yaliyokusanywa bila ya uthibitisho wa kupelekwa benki katika halmashauri hiyo ni Sh47.7 milioni, kati ya hizo Sh20.1 milioni zimerudishwa. 

Hata hivyo, Wangabo amesema taarifa za mfumo wa ukusanyaji wa mapato hadi Mei 31, 2020 unaonesha makusanyo ambayo hayajapelekwa benki yamefikia Sh53.8 milioni.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Suleiman Jafo hivi karibuni katika ziara yake mjini Sumbawanga alimtaka Mkuu huyo wa Mkoa kutumia vyombo alivyonavyo kushughulika na wadaiwa wa fedha za makusanyo ambazo hazikuwasilishwa benki.

Katika halmashauri 185 zilizokaguliwa na CAG, halmashauri 176 zilipata hati inayoridhisha na tisa zilipata hati yenye shaka ikiwemo Halmashauri ya Nkasi.

Halmashauri zilizopata hati yenye shaka zimepoteza sifa za kupatiwa fedha za utekelezaji wa miradi ya kimkakati katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
27 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
27 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
27 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Dk Nchimbi afukuzwa CCM, Ndejembi akipendekezwa kuchukua mikoba

Dk Nchimbi afukuzwa CCM, Ndejembi akipendekezwa kuchukua mikoba

Nukta TV

Haya hapa mafao ya Dk Emmanuel Nchimbi aking’atuka madarakani

Haya hapa mafao ya Dk Emmanuel Nchimbi aking’atuka madarakani

Nukta TV

SIMULIZI: Namna Magufuli, Samia walivyoichonga historia ya Bwawa la Mwalimu Nyerere

SIMULIZI: Namna Magufuli, Samia walivyoichonga historia ya Bwawa la Mwalimu Nyerere

Nukta TV