Filamu ya ‘Binti’ yaibua vipaji vipya “bongo movie”
- Ni filamu ambayo imeongelea maisha ya mwanamke wa Kitanzania kwa herufi kubwa
- Imesheheni mafunzo ya familia, mahusiano na utafutaji wa mwanamke.
- Imetambulisha sokoni vipaji vipya katika tasnia ya uigizaji.
Dar es Salaam. Bila shaka kuna mambo mengi yanayokusubiri kufanya hasa kama ni mwanamke katika jamii ya Kiafrika. Wanawake wanaweza kulijibu na kulithibitisha jambo hilo.
Kwa mwanamke, utalazimika kufanya mengi ikiwemo kulea familia, kufanya kazi ili kuchangia kipato cha familia, kupingana na mfumo dume ili kufikia malengo yako bila kutumia mwili wako na mengine mengi ambayo wanawake hawasimulii.
Hayo yote yamekuwa ni sehemu ya masuala yaliyoandikwa kwa herufi kubwa katika filamu ya inayoendwa kwa jina la “Binti” ambayo inaonyesha hadithi ya upambanaji wa wanawake wanne wanaolazimika kufanya mapinduzi ya maisha yao.
Filamu hiyo iliyosheheni nyota wageni katika tasnia ya filamu Tanzania wakiwemo Godliver Gordian, Helen Hartman, Jonas Mugabe na Bertha Robert imetengenezwa chini ya Seko Shamte, mwana dada ambaye ndiye mwandishi na kiongozi wa filamu hiyo.
Soma zaidi:
“Binti” imesheheni mafundisho ya unyanyapaa wa watoto wanaoishi na mahitaji maalumu, changamoto za mahusiano na mapambano ya wanamke katika kujikwamua kiuchumi.
Kwa muda, filamu hiyo imekuwa ikionyeshwa katika kumbi za kuangalizia filamu za Century Cinemax na jana ilikuwa ni tamati ya filamu hiyo katika kumbi hizo.
Hata hivyo, filamu hiyo inaendelea kuonyeshwa katika skrini za sinema mbalimbali nchini Tanzania ikiwemo Regalz Cinemax ya Arusha.
Shamte ameiambia Nukta kuwa, mwisho wa filamu hiyo kuonyeshwa katika skrini za Century Cinemax ulikuwa ni jana (Aprili 15) lakini yeye na timu yake wanapambana kuongezewa muda ili kuwafikia watu wengi kwa sababu imeonyesha muitikio mzuri.
Unasubiri kuitazama filamu hii ya kitanzania yenye mengi yatakayokuacha mdomo wazi. Ujachelewa changamkia fursa hiyo tazama kionjo cha filamu hiyo hapa:
Latest
