Mama mzazi wa Hayati Magufuli afariki dunia, Rais Samia amlilia

May 25, 2026 11:18 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Amefariki dunia leo Mei 25, 2026 nyumbani kwake Chato, mkoani Geita baada ya kuugua muda mrefu.

]Arusha. Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mama mzazi wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, Dk John Pombe Magufuli aliyefariki dunia leo Mei 25, 2026 nyumbani kwake Chato, mkoani Geita.

Jesca Magufuli, mtoto wa Hayati Magufuli amethibitisha kutokea kwa kifo hicho katika mahojiano yake na AyoTV yaliyofanyika kwa njia ya simu akifafanua kuwa bibi yake amefariki baada ya kuugua muda mrefu.

“Bibi yetu (Suzana Mussa) amefariki saa moja nyumbani kwake Chato baada ya kuugua kwa muda mrefu, taratibu za msiba familia itawajulisha, Bwana ametoa na Bwana ametwaa” amesema Jesca.

Kupitia taarifa ya Bakari Machumu, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu iliyotolewa usiku leo Maei 25,2026 imeeleza kuwa Rais Samia ametoa pole kwa familia ya Hayati Dk Magufuli, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na msiba huu.

“Kwa niaba ya Serikali, na kwa niaba yangu binafsi, naungana na familia katika kipindi hiki kigumu cha majonzi, tukiwaombea nguvu, faraja na uvumilivu…Halikadhalika, Rais Dkt. Samia anaiombea roho ya marehemu pumziko la milele. Amina,” imeeleza taarifa ya Rais Samia.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV