Yakuzingatiwa kwa watumiaji wa pombe wakati wa Uviko-19
Dar es salaam. Wakati mapambano ya Uviko-19 yakiendelea ni muhimu kwa watumiaji wa pombe kuzingatia mambo mbalimbali ya kiafya ili kutojiweka katika hatari ya kuambukizwa ugonjwa huo.
Mambo hayo ni pamoja na kuepuka unywaji wa pombe uliokithiri kwani pombe inaweza kusababisha kutofikiri vizuri hivyo kupunguza umakini wa kuchukua tahadhari dhidi ya Uviko-19.
Vile vile inashauriwa  kutokunywa  pombe saa nne hadi nane kabla na baada ya kuchanja chanjo ya Uviko-19.
Ikumbukwe kuwa  unywaji wa pombe hauui wala hauupatii mwilikinga dhidi ya virusi vya Uviko-19.

Latest