Tanzania yapokea dozi 115,200 za chanjo ya Janssen

December 3, 2021 2:26 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Tanzania imepokea shehena ya chanjo ya aina ya Janssen dozi 115,200 kutoka Serikali ya Ubeligiji kupitia mpango wa COVAX Facility itakayosaidia kuimarisha mapambano ya Uviko-19 nchini.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Dorothy Gwajima amesema kuwa Serikali itaendelea kutoa chanjo dhidi ya Uviko-19 katika vituo mbalimbali vya afya ili kuwakinga wananchi.

Dozi hizo zimepokolewa katika uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam kutoka kwa Balozi wa Ubeligiji nchini Tanzania, Peter Van Acker.

Kwa mujibu wa Dk Gwajima, awamu ya kwanza Serikali ilipokea dozi milioni 1.05, awamu ya pili dozi 169,000 na leo Desemba 3, 2021 imepokea 115,200 hivyo kufanya jumla ya Chanjo aina ya Janssen zilizopokelewa hapa nchini kufikia dozi milioni 1.34.

Hiyo inafanya jumla ya chanjo zote zilizopokelewa nchini mpaka sasa kufikia dozi milioni 4.42 zikiwemo chanjo ya Sinopharm na Pfizer ambazo zitachanja watu milioni 2.88. 

Aidha, Dk Gwajima amewaagiza viongozi na watendaji wa ngazi zote kutoa ushirikiano wa hali ya juu na kuhamasisha jamii kujitokeza kupata chanjo na  kisha kujikinga kwa kuchukua tahadhari dhidi ya Uviko 19. 

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW