Kinga ni bora kuliko tiba: Serikali ya Tanzania yaongeza kasi chanjo ya Corona

September 29, 2021 1:05 pm · Herimina
Share
Tweet
Copy Link
  • Idadi ya vituo vya kutolea chanjo ya Uviko-19 yaongezwa.
  • Ikiwa ni hatua ya serikali katika kurahisisha upatikanaji wa chanjo hiyo.

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imeongeza juhudi katika kuongeza ushiriki wa wananchi katika kuchanja chanjo ya Uviko-19, ikiwa ni moja ya hatua za kuongeza idadi ya watu kuchanjwa ili kupambana na janga la Corona nchini. 

Tangu kampeni ya kutoa chanjo ya Uviko-19 ianze mwanzoni mwa Agosti 2021, dozi 400,000 zimetolewa hadi Septemba 26 kati ya zaidi ya milioni aina ya Johnson & Johnson zilizoingizwa nchini kupitiz mpango wa Covax. Kiwango hicho ni asilimia 38 ya dozi zote za chanjo zilizopokelewa Tanzania. 

Katika kuongeza hamasa ya watu kujitokeza kuchanja, Tanzania imeongeza juhudi za kuwafikia watu wengi zaidi ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya vituo vya kutolea chanjo hiyo kutoka vituo 550 hadi vituo 6,784 ili kurahisisha upatikanaji wa huduma hiyo.Vilevile, Serikali imeongeza uhamasishaji na utoaji elimu kwa wananchi kuhusu chanjo ya Uviko-19 kupitia kampeni ya nyumba kwa nyumba.

Katika hatua nyingine, Serikali ya Tanzania inakamilisha taratibu za kuleta chanjo nyingine aina ya ‘Sinopharm’ dozi milioni 2 kutoka nchini China, idadi itakayofanya jumla ya chanjo zilizopokelewa kufikia milioni 3.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
18 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
18 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Nukta TV

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Nukta TV

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Nukta TV