Wafuasi 34 wa Mfalme Zumaridi wapata dhamana
- Ni baada ya wakili wao kuwasilisha ombi mahakamani.
- Walioachiwa mpaka sasa kwa dhamana ni 75.
- Mfalme Zumaridi aendelea kusota rumande.
Mwanza. Kesi inayomkabili Diana Bundala maarufu kama “Mfalme Zumaridi” na wafuasi wake 93 imesomwa tena leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza huku washtakiwa wengine 34 wakipatiwa dhamana na kufanya jumla yao kufikia 75.
Washtakiwa wengine 17 wanaendelea kusota rumande pamoja na kiongozi wao hadi kesi hiyo namba 10,11 na 12 itakapotajwa tena Machi 31, 2022.
Hatua hiyo imefikiwa baada ya Wakili wa Utetezi, Erick Mutta kuwawasilisha barua 34 za ombi la dhamana kwa wateja wake ambapo hakimu Monica Ndyekobora akaridhia dhamana.
Zumaridi na washtakiwa 17 wamerejshwa Gereza Kuu Butimba na wanatarajia kuungana na wenzao waliopewa dhamana Machi 31, 2022 kesi zao zitakaposomwa tena.
Soma zaidi:
‘Mfalme’ Zumaridi kufikishwa mahakamani
Wakisomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Monica Ndyekobora, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Doecas Ankyoo ametaja kesi hiyo na mashtaka yao ambayo ni usafirishaji haramu wa binadamu inayomkabili Zumaridi pekee.
Kesi namba 11 ya shambulio la kudhuru mwili na kuzuia maafisa wa Serikali kutekeleza majukumu yao inayowakabili Zumaridi na wenzake nane huku kesi na 12 ni kusanyiko lisilokua halali inayowaweka kitanzini Zumaridi na wafuasi wake 84.
Katika kesi hiyo, Serikali imewakilishwa na Wakili Dorcas Ankyoo ambaye aliishia kuitaja tu kesi namba 10 inayomkabiri Zumaridi pekee na kutokana na mahakama kutokuwa na mamlaka ya kisheria kuisikiliza shauri hilo Hakimu Ndyekobora akaipangia March 31, 2022.
Katika kesi namba 11 na 12, Wakili Ankyoo amesema upepelezi umekamilika na akaomba tarehe nyingine ipangwe kwa ajili ya kusikiliza hoja za awali na hakimu Ndyekobora akaipaga March 31, 2022.
Latest