Fahamu mishahara mipya ya wafanyakazi wa ndani, hotelini

December 6, 2022 2:51 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Dar Dar es Salaam. Serikali imetangaza viwango vipya vya kima cha chini cha mishahara kwa wafanyakazi wa ndani na hotelini ambavyo vitaanza kutumika Januari 1, 2023.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,  Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako katika tangazo lilitolewa katika Gazeti la Serikali, amesema viwango hivyo ni kwa sekta binafsi. 

Viwango hivyo vitawanufaisha zaidi wafanyakazi wa kazi za ndani wale wasioajiriwa na wanadiplomasia, wafanyabiashara wakubwa na maafisa wenye stahiki ambapo watakuwa wanalipwa Sh60,000 kwa mwezi kuanzia mwaka ujao. 

Kiwango hicho kimeongezeka kutoka Sh40,000 waliyokuwa wakilipwa hapo awali kwa mujibu wa Takwimu muhimu za Tanzania za mwaka 2018 zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).

Wafanyakazi wa ndani wanaoilipwa kima cha chini cha mshahara cha juu kuliko wengine ni wale wafanyakazi wa kazi za ndani walioajiriwa na wanadiplomasia na wafanya biashara wakubwa. Kwa mujibu wa tangazo hilo watalipwa Sh250,000. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV