Watahiniwa 393 wafutiwa matokeo darasa saba, idadi ikipungua

October 30, 2021 2:11 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni waliofanya mtihani wa kuhitimu darasa la saba mwaka 2021.
  • Idadi hiyo imepungua kutoka 1,059 waliofutiwa mwaka 2020.
  • Necta yashauri wachukuliwe hatua kwa vitendo vya udanganyifu wa mitihani.

Dar es Salaam. Watahiniwa 393 waliofanya mtihani wa kuhitimu darasa la saba mwaka 2021 wamefutiwa matokeo yao baada ya kubainika kufanya udanganyifu katika mitihani huo. 

Mtihani huo ulifanyika Septemba 8 na 9 mwaka huu na matokeo yake yametangazwa leo jijini Dar es Salaam na Baraza la Mtihani Tanzania (NECTA) na kuonyesha ufaulu wa jumla wa wanafunzi umefikia asilimia 81.97. 

Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk Charles Msonde amewaambia wanahabari kuwa wamebaini vitendo vya udanganyifu katika mtihani huo uliofanyika na wamechukua hatua ya kufuta matokeo ya watahiniwa hao 393.

Dk Charles Msonde amesema baraza limezishauri mamlaka husika kuwachukulia hatua waliohusika na udanganyifu huo ikiwemo kuwafikisha katika vyombo vya sheria.

“Baraza limezishauri mamla kuwachukulia hatua wale wote waliohusika kwa namna moja au nyingine kusababisha kutokea  kwa udanganyifu katika mitihani” amesema Dk Msonde.

Hata hivyo, idadi ya watahiniwa waliofutiwa matokeo mwaka huu imepungua kwa asilimia 62.8 kutoka watahiniwa 1,059 waliofutiwa mwaka 2020.

Pia Necta imezuia kutoa matokeo ya watahiniwa 128 ambao waliugua au kupata matatizo na kushindwa kufanya mtihani kwa masomo yote au baadhi ya masomo.

Dk Msonde amesema watahiniwa hao wamepewa fursa nyingine ya kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2022 kwa mujibu wa kifungu 32(1) cha kanuni za mitihani.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Nukta TV

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

Nukta TV

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV