Yaliyojiri bajeti ya Wizara ya Maendeleo na Vijana ikisomwa kwa mara ya kwanza

April 20, 2026 4:40 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Vipaumble, changamoto na mikakati ya kuwainua vijana ni miongoni mwa yalijadiliwa.

 Dar es Salaam. Bajeti ya Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana imesomwa kwa mara ya kwanza Bungeni Dodoma leo Aprili 20, 2026 tangu kuanzishwa rasmi kwa wizara hiyo na Rais Samia Suluhu Novemba 17 mwaka jana.

Akiwasilisha bajeti hiyo leo Aprili 20, 2026 bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Joel Nanauka ameliomba Bunge liidhinishe Sh35.9 bilioni kwa mwaka wa fedha 2026/27 ili kutekeleza shughuli mbalimbali za wizara hiyo.

Awali masuala ya vijana yalikuwa yakishuguhulikiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu chini ya Waziri Ridhiwani Kikwete

Kwa mujibu wa Rais Samia lengo la kuanzisha wizara hiyo ni kuhakikisha vijana wanapata jukwaa la kusikika na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi.

Pamoja na kuanzishwa kwa wizara hiyo Rais Samia aliahidi  kuanzisha kitengo cha washauri wa vijana ndani ya ofisi ya Rais.

Akizungumza leo Aprili 20, 2026 bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Joel Nanauka, ameeleza kuwa kati ya bajeti hiyo inayosubiri kuidhinishwa na Bunge Sh30.1 bilioni zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

Katika kiasi hicho cha matumizi hayo ya kawaida, Sh1.22 bilioni ni kwa ajili ya mishahara, huku Sh28.8 bilioni zikiwa kwa matumizi mengineyo (OC). 

Kwa upande mwingine Sh5.85 bilioni zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ambapo Sh5 bilioni ni fedha za ndani na Sh853.03 milioni ni fedha za nje.

Aidha, Nanauka amesisitiza ukubwa na umuhimu wa kundi la vijana nchini, akibainisha kuwa zaidi ya vijana milioni 20, sawa na asilimia 34.4 ya Watanzania, wanachangia zaidi ya asilimia 55 ya nguvu kazi ya taifa. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV