Wizara ya Afya: kuchangia figo ni bure

September 2, 2025 5:55 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni ndugu wa karibu pekee ndiye anayeruhusiwa kuchangia figo na mchango huo unafanyika bila malipo yoyote.

Dar es Salaam. Serikali imesema huduma ya kuchangia figo kwa wahitaji wa matibabu hayo ni bure na haifanyiki kibiashara kama ambavyo inaelezwa kwenye taarifa mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii.

Taarifa ya Aminiel Aligaesha, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa Hospitali ya Muhimbili, iliyotolewa leo Septemba 2 ,2025 imeeleza kuwa huduma ya kuchangia figo katika hospitali hiyo inafanywa na ndugu wa mgonjwa husika bila malipo na sio kibiashara.

Kwa mujibu wa Aligaesha Kabla ya mchangiaji kuchangia, kamati ya uidhinishaji inayojumuisha wanasheria, viongozi wa dini, madaktari na maafisa ustawi wa jamii, hupitia maombi ya upandikizaji, kufanya mahojiano na wahusika pamoja na kuthibitisha uhusiano wao kupitia nyaraka muhimu ikiwemo vyeti vya kuzaliwa, viapo, picha na vipimo vya kitabibu.

“Uchangiaji  wa figo unaofanyika nchini Tanzania unasimamiwa na Kanuni za Huduma za Figo za mwaka 2017 zilizopitishwa na Wizara ya Afya kwa kuzingatia miongozo na maazimio ya kimataifa ambayo yanakataza biashara ya viungo vya binadamu,” imeeleza taarifa ya Muhimbili.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, jumla ya wagonjwa 106 wamenufaika na huduma ya kupandikiza figo tangu ilipoanzishwa  Septemba 2017.

Hata hivyo, taarifa hiyo haijafafanua hatua za kisheria zitakazochukuluwa dhidi ya watoa huduma za afya na wananchi watakaoshiriki katika uuzaji au usafirishaji wa kiungo hicho muhimu mwilini kwa mwanadamu.

Muhimbili imesisitiza kuwa itaendelea kutoa huduma hizo kwa kuzingatia kanuni na kufuata viwango vya kimataifa ili kulinda afya na usalama wa wagonjwa pamoja na wachangiaji.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV