Waziri Kigwangalla: Kazi ya kuzima moto uliozuka Mlima Kilimanjaro ni ngumu

October 15, 2020 5:57 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Amesema kazi ya kuzima moto uliozuka mwishoni mwa wiki ni ngumu na kubwa kuliko inavyodhaniwa.
  • Ugumu huo unasababishwa na upepo mkali na kukauka kwa nyasi na vichaka. 
  • Helikopta na ndege kuanza kutumika kuzima moto huo ikiwa taratibu zitakamilika leo.

Dar es Salaam. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla amesema kazi ya kuzima moto uliozuka Mlima Kilimanjaro mwishoni mwa wiki ni ngumu na kubwa kuliko inavyodhaniwa kwa sababu ya changamoto ya upepo mkali na kukauka kwa nyasi na vichaka. 

Moto huo ulizuka Jumapili Oktoba 11, 2020 katika eneo la Whona ambacho ni kituo cha kupumzikia wageni wanaotumia njia ya Mandara na Horombo kupanda mlima huo mrefu kuliko yote Afrika.

“Bado tunahangaika na kuzima moto. Kazi ni ngumu na kubwa kuliko inavyodhaniwa. Changamoto ni upepo mkali na kukauka kwa nyasi na vichaka,” ameandika Dk Kigwangalla katika ukurasa wake wa Twitter leo (Oktoba 15, 2020).

Amesema kutokana na hali hiyo, wanakusudia kutumia helikopta na ndege kudhibiti moto huo.

“Taratibu zikikamilika leo tutaweza kuanza kutumia helikopta na ndege kuzima moto,” amesema Waziri huyo.

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Mawasiliano wa Tanapa, Pascal Shelutete katika taarifa yake iliyotolewa Oktoba 13, 2020 alisema kazi ya  helikopta hiyo itakuwa ni kuangalia eneo lililoathirika na kufuatilia maeneo mengine yanayoweza kushika moto.

Amesema jumla ya nguvukazi ya watu 500 wako eneo la tukio kukabiliana na moto huo ambao kwa sehemu kubwa tayari umedhibitiwa. 


Soma zaidi:


Hata hivyo, Tanapa imesema inachukua tahadhari zote ili kuhakikisha usalama wa wageni na vifaa vyao unaimarika bila kuathiri shughuli za utalii ambazo zinaendelea kama kawaida hususan njia ya Marangu iliyoathirika na moto husika.

Mamlaka zinaeleza kuwa wastani wa watu 50,000 hupanda mlima huo kila mwaka.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV