Wafanyabiashara waonywa kupandisha bei ya vyakula msimu wa Ramadhani, Kwaresma

January 29, 2026 12:58 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Waziri asema akiba ya chakula nchini inajitoshereza.
  • Awahimiza wananchi kutumia chakula kwa uangalifu, kutunza akiba na kuepuka matumizi yasiyo ya lazima.

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imewaonywa wafanyabiashara nchini kuacha kutumia miezi ya Ramadhani na Kwaresima kama kisingizio cha kupandisha bei za vyakula suala linaloacha maumivu kwa wananchi.

Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba aliyekuwa akizungumza wakati wa kipindi cha maswali na majibu bungeni leo Januari 29, 2026 amesisitiza kuwa Taifa lina akiba ya kutosha ya chakula hivyo wafanyabiashara hawapaswi kupandisha bei.

Nitoe rai kwa wafanyabiashara wasitumie vipindi hivi vya Kwaresma na Mwezi mtukufuu wa Ramadhani kujipatia faida iliyopitiliza viwango na kuwaumiza Watanzania kwa kisingizio cha tahadhari ya Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA),” amesisitiza Waziri Mkuu.

Si mara ya kwanza kwa Serikali kutoa wito kwa wafanyabiashara kuacha kupandisha bei za bidhaa, hususan vyakula, kila inapokaribia miezi ya mifungo ya kidini kama Ramadhani na Kwaresma.

Mifungo hiyo inayotarajiwa kuanza kati ya Februari 17 na 18 kwa Waislamu na baadhi ya Wakristo duniani, inalenga kuwakumbusha waumini umuhimu wa misingi ya imani zao, sambamba na kuhimiza mshikamano na kuwajali watu wenye kipato cha chini.

Tanzania inajitosheleza kwa chakula

Dk Nchemba amekiri uwepo wa ufinyu wa mvua unaochangiwa na mabadiliko ya hali ya hewa yaliyotangazwa na TMA siku za hivi karibuni akiwahakikishia Watanzania kuwa chakula kipo cha kutosha hivyo hakuna sababu ya kupandisha bei za vyakula.

““Kwa sasa tuna chakula cha kutosha. Mahitaji ya akiba ya chakula kitaifa ni takribani tani 150,000…

…Nchi ina zaidi ya tani 400,000 za akiba. Kati ya hizo, tani 150,000 ni kiwango cha kawaida na zaidi ya tani 200,000 ni ziada,” alisema Waziri Mkuu akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa, Nancy Hassan Nyalusi.

Kuanzia Septemba 2025 TMA  imekuwa ikiwatahadharisha wananchi juu ya uwezekano wa kunyesha kwa mvua pungufu, hali inayoweza kuathiri ukuaji wa mazao na kusababisha wakulima kuvuna mazao machache kuliko ilivyotarajiwa.Pamoja na uwepo wa changamoto hiyo, Serikali imesema itaendelea kuwahamasisha wakuu wa mikoa na wilaya kutoa elimu kwa wananchi, hususan katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua chache, ili wapande mazao yanayostahimili ukame na yanayoweza kukomaa kwa kutegemea mvua zisizo na mtawanyiko mzuri.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV