Vyakula vinavyowafaa wanaosumbuliwa na vidonda vya tumbo
- Ni pamoja na matunda na mboga za majani.
- Bado unashauriwa kumuona daktari ili upate maelekezo sahihi zaidi.
Dar es Salaam. Vindonda vya tumbo (Ulcers) ni changamoto ya kiafya ambayo husababishwa na mambo mengi ikiwemo aina ya vyakula na baadhi ya dawa zinazotumiwa na watu mara kwa mara.
Matahalan, kwa mtu anayetumia pilipili, baadhi ya vinywaji kama kahawa bila ulinganifu, yupo katika hatari ya kusumbuliwa na ugonjwa huu.
Kwa mujibu wa Kathryn Watson anayeandikia tovuti ya afya ya Healthline, baadhi ya vyakula vinavyoweza kumsababishia mtu kupata vidonda vya tumbo ni pamoja na vyakula vilivyoshamiri viungo (spices), matumizi ya vyakula vya jamii ya malimao (citrous), pilipili na matumizi ya baadhi ya dawa zikiwemo ‘aspirin’ na ‘ibuprofen’.
Kwa mazingira ya Kitanzania, vyakula gani vitamsaidia mtu aliye na vidonda vya tumbo? Tazama video hii kujifunza:
Latest
