UNICEF yaonya kuongezeka ndoa za utotoni duniani

March 10, 2021 6:12 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Imeonya kuwa huenda kukawa na ndoa za utotoni milioni 10 kabla ya kumalizika kwa muongo huu.
  • Changamoto za kiuchumi, kuingiliwa kwa huduma, mimba na vifo vya wazazi kutokana na janga la COVID-19 kutachangia ongezeko hilo.
  • UNICEF inataka hatua madhubuti zichukuliwe sasa kabla hali haijawa mbaya zaidi. 

Ripoti ya mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) imeonya kuwa huenda kukawa na ndoa za utotoni milioni 10 kabla ya kumalizika kwa muongo huu na hivyo kutishia mstakabali wa elimu ya wasichana duniani. 

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyopewa jina “COVID-19: tishio kwa hatua zilizopigwa dhidi ya ndoa za utotoni”, kufungwa kwa shule, changamoto za kiuchumi, kuingiliwa kwa huduma, mimba na vifo vya wazazi kutokana na janga la COVID-19 vinawaweka wasichana walio katika mazingira magumu katika hatari ya ndoa za utotoni. 

Ripoti imesema kuwa hata kabla ya COVID-19 wasichana milioni 100 walikuwa katika hatari ya ndoa za utotoni katika kipindi cha miaka 10 ijayo  licha ya ndoa hizo kupungua kwa kiasi kikubwa katika baadhi ya nchi kwa  miaka ya hivi karibuni, kwa asilimia 15.

Kupungua kwa ndoa hizo ni sawa na ndoa milioni 25 zilizoepushwa, lakini sasa mafanikio hayo yanaweza yasifikiwe kikamilifu.  


Zinazohusiana:


Ripoti hiyo inasema wasichana wengi ambao wanaoolewa utotoni wanakabiliwa na changamoto lukuki za muda mfupi na za muda mrefu na wengi hukumbana na ukatili na pia kukatiza masomo.

Inaelezwa na ripoti hiyo kuwa janga la COVID-19 limezidisha adha ya ndoa hizo na duniani kote inakadiriwa kuwa wanawake na wasichana milioni 650 walio hai leo hii wamepitia ndoa za utotoni na nusu ya ndoa hizo zikitokea Bangladesh, Brazil, Ethiopia, India na Nigeria. 

 Hivyo UNICEF inataka hatua madhubuti zichukuliwe sasa kabla hali haijawa mbaya zaidi. 

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV