Umoja wa Ulaya kuanza kutumia chanja aina moja za simu
- Lengo ni kutunza mazingira na kurahisisha upatikanaji wake.
- Zitaanza kutumiaka mwaka 2024 katika nchi zote za umoja huo.
- Sheria itaanza kutumika rasmi 2024.
Dar es salaam. Dar es Salaam. Umoja wa Ulaya (EU) umepitisha azimio la kutumia chaja zinazofahamika kama ‘type C’ kwenye simu zote pamoja na vifaa vya umeme vya kuchajiwa vitakavyouzwa ndani ya umoja huo ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira.
EU imesema mchaja hizo zitasaidia kupunguza uchafu wa taka za kielektroniki pamoja na kurahisisha maisha ya watumiaji.
Bunge la EU limeeleza kuwa chini ya sheria mpya, watumiaji wa chaja aina C hawatalazimika kuwa na chaja tofauti tofauti za vifaa vya umeme wala kununua chaja pale wanaponunua vifaa vipya kwani chaja moja inaweza kutumika kwenye vifaa tofauti.
Taarifa ya bunge hilo iliyotolewa Juni 7, 2022 imebainisha kuwa utekelezaji wa sheria hiyo unaotarajiwa kuanza mwaka 2024 na utasaidia kuokoa kiasi cha Euro milioni 250 (Sh6.4 trilioni) kutokana na manunuzi yasiyo ya lazima ya chaja.
Soma zaidi:
- Jinsi ya kufanya mitandao ya kijamii isikuharibie mahusiano yako
- Mbinu tano za kudhibiti matumizi makubwa ya intaneti kwenye ‘smartphones’
Makampuni ya utengenezaji wa vifaa vya kielektroniki kama vile simu za mkononi, kamera, vishikwambi na spika za masikioni wataanza kutekeleza sheria hiyo mwaka 2024 huku wakijiandaa na mabadiliko ya chaji za kompyuta mpakato katika miezi 40 ijayo.
Hali itakuaje kwa watumiaji wa iPhone?
Kamisheni ya Umoja wa Ulaya inaeleza kuwa mwaka 2020 takribani chaji milioni 450 ziliuzwa kaika umoja huo ambapo karibu theluthi mbili ya watumiaji walipatwa na changamoto za kimatumizi
Kamisheni hiyo inaeleza kuwa katika muongo uliopita umefanikiwa kupunguza idadi ya chaja za simu kutoka 30 mpaka tatu, ingawa changamoto kubwa ipo kwa watumiaji wa bidhaa za Iphone ambazo ni karibu na asilimia 20 za soko la bidhaa za kielektroniki barani Ulaya.