Tunachokifahamu kuhusu ujenzi wa soko jipya la Kariakoo

April 15, 2023 8:04 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Hadi Februari mwaka huu Sh4.16 bilioni zimepokelewa kwa ajili ya ujenzi wa soko la Kariakoo.
  • Ujenzi wa soko hilo umefikia hatua ya kumwaga jamvi la ghorofa ya tano kati ya ghorofa sita.
  • Litakamilika Oktoba 2023 na kuchukua wafanyabiashara 2,300. 

Dar es Salaam. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Angellah Kairuki amesema hadi kufikia Februari mwaka huu Sh4.16 bilioni zimepokelewa kwa ajili ya ujenzi wa soko la Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Serikali ilitoa Sh10 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa Soko la Kariakoo unaohusisha ujenzi wa jengo jipya na ukarabati wa jengo la soko la zamani lililoungua Julai 2021. 

“Hadi Februari, 2023, Sh4.16 bilioni zimepokelewa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu, sawa na asilimia 42 ya fedha zilizoidhinishwa,” amesema Kairuki wakati akiwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha wa 2023/24 bungeni jijini Dodoma Aprili 14. 

Ujenzi wa soko hilo unaojengwa na kampuni ya Estim Construction Ltd umefikia hatua ya kumwaga jamvi la ghorofa ya tano kati ya ghorofa sita ikihusisha ghorofa mbili za chini ya ardhi (basement). 

Ukarabati wa jengo la zamani unaendelea na umefikia asilimia 62.

Soko Kuu la Kariakoo liliungua Julai 10, 2021 usiku huku  wafanyabaishara 224 wakipoteza bidhaa zao. Serikali haikuwaruhusu wafanyabiashara kurudi tena na badala yake ilianza mchakato wa ujenzi wa soko jipya na ukarabati wa jengo la zamani. 


Soma zaidi:


Manufaa ya soko hilo

“Kukamilika kwa ujenzi na ukarabati wa soko hili kutachochea ukuaji wa biashara katika Jiji la Dar es Salaam, mikoa mingine na nchi jirani,” amesema Kairuki kuhusu soko hilo ambalo ni kiungo cha biashara Tanzania na nchi jirani. 

Ujenzi wa soko hilo unataraijwa kukamilika Oktoba, 2023 na litakapokamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua wafanyabiashara 2,300 sawa na ongezeko la wafanyabiashara 638 ukilinganisha na wafanyabiashara 1,662 waliokuwepo kabla ya ukarabati wa jengo la zamani na ujenzi wa jengo jipya. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.