TRC yarejesha safari za treni za SGR

October 23, 2025 3:29 pm · Esau Ng'umbi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya kukamilika kwa matengenezo ya mufa mfupi yaliyofanyika.

Dar es Salaam. Shirika la Reli Tanzania (TRC) limerejesha safari za treni za umeme za SGR, baada ya kusitisha kwa muda leo.

Hatua hiyo imekuja baada ya matengenezo ya muda mfupi yaliyofanyika, kutokana na treni ya Electric Multiple Unit – EMU maarufu mchongoko iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma leo Alhamisi Oktoba 23, 2025 kupata ajali katika kituo cha Ruvu mkoani Pwani.

Taarifa kwa umma iliyotolewa mchana huu na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano TRC, Fredy Mwanjala imeeleza kuwa safari sasa zinaendelea kama kawaida.

“Shirika la Reli Tanzania linapenda kuujulisha umma kuwa huduma za usafiri wa treni za SGR zimerejea na kuendelea kama kawaida. Shirika linaomba radhi wateja wake kwa usumbufu uliojitokeza na pia linawashukuru kwa uvumilivu wao.

Huduma bora kwa wateja wetu ndiyo kipaumbele cha Shirika,” imeeleza taarifa hiyo.

Awali taarifa iliyotolewa na Shirika la Reli Tanzania (TRC) kwa umma ilitaja chanzo cha awali cha ajali hiyo kuwa ni  hitilafu za kiuendeshaji.

Hata hivyo, hakuna kifo kilichoripotiwa kutokana na ajali hiyo.

Treni ya mchongoko, ambayo imekuwa ikifanya safari zake kutoka Dar es Salaam, Morogoro hadi Dodoma ilianza kutoa huduma Novemba Mosi, mwaka 2024.

Hii ni ajali ya kwanza iliyohusisha mabehewa matatu kuhama nje ya reli, awali zilikuwa zikiripotiwa hitilafu zinazodaiwa kuwa za umeme ambapo safari zilikuwa zikisimama kupisha matengenezo na kisha safari kuendelea.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV