TRC: Hitilafu ya kiuendeshaji chanzo ajali ya SGR

October 23, 2025 11:30 am · Esau Ng'umbi
Share
Tweet
Copy Link
  • Yasema uchunguzi wa kina na juhudi za kuhakikisha kwamba huduma zinarejea haraka zinaendelea 

Dar es Salaam. Shirika la Reli nchini  (TRC) limesema hitilafu ya kiuendeshaji ndoo chanzo cha ajali ya treni ya umeme iliyokua ikisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma majira ya saa 2:00 asubuhi leo Oktoba 23, 2025 .

Ajali hiyo  imetokea kituo cha Ruvu na kwa taarifa za awali hakuna tukio la kifo.

Taarifa ya TRC iliyotolewa na Mkurugeni Mkuu Mhandisi Machibya Shiwa, imeeleza kuwa kwa sasa timu ya wataalamu ikiongozwa na Katibu Mkuu Uchukuzi,  vyombo vya ulinzi na usalama na menejimenti ya TRC inaendelea na uchunguzi wa kina na juhudi za kuhakikisha kwamba huduma zetu zinarejea haraka

Aidha, TRC imeomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kwa abiria kutokana na ajali hiyo.

Hii ni ajali ya kwanza iliyohusisha mabehewa matatu kuhama nje ya reli, awali zilikuwa zikiripotiwa hitilafu zinazodaiwa kuwa za umeme ambapo safari zilikuwa zikisimama kupisha matengenezo na kisha safari kuendelea.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...

Enable Notifications OK No thanks