TMA yaotoa tahadhari mvua na radi siku 10 mfululizo

January 2, 2026 3:38 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Yawataka wananchi kuchukua tahadhari stahiki ili kuepuka hatari zinazoweza kusababishwa na mvua hizo.

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetabiri uwepo wa mvua zinazoambatana na ngurumo za radi katika maeneo mbalimbali ya nchi kuanzia Januari 1 hadi 10, 2026 ikiwataka wananchi kuchukua tahadhari.

Kwa mujibu wa taarifa ya TMA iliyotolewa leo Januari 2, 2026, mvua hizo zinatarajiwa kunyesha katika mikoa ya Ukanda wa Ziwa Viktoria ambayo ni Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara. 

“Mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zinatarajiwa katika maeneo machache hususan katika kipindi cha siku tano za mwanzo” imeeleza taarifa hiyo.

Taaarifa hiyo ya TMA ni muendelezo wa tahadhari inayoendelea kutolewa kuanzia Desemba 11 mwaka jana ikichangiwa zaidi na mvua za msimu zilizotabiriwa kuanza Novemba 2025 hadi Aprili 2026. 

Kwa upande wa Magharibi mwa nchi, mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora inatarajiwa kupata mvua zinazoambatana na ngurumo za radi katika baadhi ya maeneo. 

Nyanda za Juu Kusini-Magharibi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa pia zinatarajiwa kupata mvua hizo katika maeneo machache pamoja na mikoa ya nyanda za juu kaskazini.

“Nyanda za juu kaskazini mashariki, mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro, itapata vipindi vya mvua vichache, hasa katika siku tano za mwanzo za Januari,” imesema taarifa ya TMA.

Vilevile, pwani ya kaskazini inayojumuisha mkoa wa Tanga, maeneo ya kaskazini mwa Morogoro, pwani ya Dar es Salaam pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba vinatarajiwa kupata vipindi vya mvua.

Kwa mujibu wa utabiri huo, mikoa ya Pwani ya Kusini, Mtwara na Lindi inatarajiwa kupata vipindi vya mvua vichache, huku Kanda ya Kusini inayojumuisha Ruvuma na maeneo ya kusini mwa Morogoro ikitarajiwa kupata mvua zinazoambatana na ngurumo za radi katika baadhi ya maeneo.

“Magharibi mwa nchi, mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora inatarajiwa kupata mvua zinazoambatana na ngurumo za radi katika baadhi ya maeneo,” imesema taarifa ya TMA.

TMA imewahimiza wananchi, hususan wakulima na wafugaji, kufuatilia taarifa za hali ya hewa na kuzingatia ratiba za mvua ili kuepuka hasara za mazao na mali, pamoja na kuchukua tahadhari dhidi ya athari za radi na mvua kubwa.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV