Rais Samia afanya uteuzi Muhimbili, BoT, TMA,TEITI

January 29, 2026 6:11 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Kati yao yupo Dk Ladislaus Benedict Chan’ga aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu TMA.

Arusha. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi wanne katika taasisi mbalimbali nchini.

Taarifa ya Bakari Machumu, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu iliyonukuu taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dk Moses Kusiluka iliyotolewa leo Januari 29, 2026 inabainisha kuwa walioteuliwa ni pamoja na Dk Rahma Salim Mahfoudh.

“Dk Mahfoudh ameteuliwa kuwa Naibu Gavana, Utawala na Udhibiti wa Ndani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) akichukua nafasi ya Julian Banzi Raphael ambaye amemaliza muda wake,” imesema taarifa ya Machumu.

Mwingine ni Dk Ladislaus Benedict Chan’ga aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) baada ya kaimu nafasi hiyo kwa kipindi kirefu.

Prof. Muhammad Bakari Kambi ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili akichukua nafasi ya Dkt. Ellen Mkondya Senkoro ambaye amemaliza muda wake.

Pamoja na hao Rais Samia pia amemteua Balozi Wilson Kajumula Masilingi kuwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia Tanzania (TEITI) akichukua nafasi ya CPA. Ludovick Utouh ambaye amemaliza muda wake.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.