Rais Samia afanya uteuzi Muhimbili, BoT, TMA,TEITI

January 29, 2026 6:11 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Kati yao yupo Dk Ladislaus Benedict Chan’ga aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu TMA.

Arusha. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi wanne katika taasisi mbalimbali nchini.

Taarifa ya Bakari Machumu, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu iliyonukuu taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dk Moses Kusiluka iliyotolewa leo Januari 29, 2026 inabainisha kuwa walioteuliwa ni pamoja na Dk Rahma Salim Mahfoudh.

“Dk Mahfoudh ameteuliwa kuwa Naibu Gavana, Utawala na Udhibiti wa Ndani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) akichukua nafasi ya Julian Banzi Raphael ambaye amemaliza muda wake,” imesema taarifa ya Machumu.

Mwingine ni Dk Ladislaus Benedict Chan’ga aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) baada ya kaimu nafasi hiyo kwa kipindi kirefu.

Prof. Muhammad Bakari Kambi ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili akichukua nafasi ya Dkt. Ellen Mkondya Senkoro ambaye amemaliza muda wake.

Pamoja na hao Rais Samia pia amemteua Balozi Wilson Kajumula Masilingi kuwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia Tanzania (TEITI) akichukua nafasi ya CPA. Ludovick Utouh ambaye amemaliza muda wake.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
25 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

Nukta TV

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV