Tanzania yazindua filamu kutangaza utalii kimataifa

May 29, 2020 2:20 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Imetafsiriwa katika lugha tano kikiwemo Kiswahili.
  • Itasaidia kuyafikia masoko ya utalii ya kimataifa na kuongeza mapato ya Taifa.
  • Watanzania watakiwa kuisambaza kwa kasi ili kuvutia watalii wengi.

Dar es Salaam. Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imezindua rasmi filamu inayoitambulisha Tanzania ndani na nje ya nchi katika maeneo mbalimbali ya utalii ikiwa ni hatua ya kuongeza wigo wa masoko kimataifa. 

Uzinduzi huo ni miongoni mwa mikakati ya TTB iliyojiwekea hivi karibuni kukabiliana na athari za ugonjwa wa virusi vya Corona katika sekta ya utalii nchini.

Waziri Mwenye wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla amesema lengo la filamu hiyo fupi ya “Tanzania Unforgettable” (Tanzania isiyosahaulika) ni kutambulisha vivutio vya utalii katika soko la utalii kimataifa.

Dk Kigwangala amewataka Watanzania kuisambaza  filamu hiyo kwenye mitandao yao ya kijamii ikiwemo Facebook, Twitter, Instagram, Telegram na mitandao mingine, ili iweze kuwafikia walengwa.

“Kwa hiyo ninaomba Watanzania wenzangu tuisambaze kwenye mitandao yetu ya kijamii kwa maana imetafsiriwa katika lugha ya Kiswahili, Kingereza, Kifaransa, Kihispania, Kiisrael na Kichina”, amesema Waziri huyo leo Mei 29.


Zinazohusiana: 


Huenda filamu hiyo ikasaidia kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Tanzania, ikizingatiwa kuwa idadi ya watalii wanaokuja nchini mwaka huu itashuka kutoka milioni 1.8 waliotarajiwa hadi kufikia watalii 437,000 kutokana n aathari za janga la Corona.

Mkurugenzi Mtendaji wa TTB Devotha Mdachi amesema kuwa Tanzania kwa sasa imejikita zaidi kutangaza vivutio vya utalii kupitia mitandao ya kijamii, kwa hiyo kuzinduliwa kwa filamu hiyo fupi kutawasaidia kuteka soko la ndani na nje ya nchi.

Amesema kupitia filamu hiyo fupi watalii watapata fursa ya kuona utamaduni na maeneo mbalimbali ya kuvutia na kuweza kuchagua sehemu sahihi ya kwenda kutembelea.

Filamu hiyo iko katika ukubwa wa dakika moja, dakika tatu, dakika saba na dakika 10 inapatikana YouTube na akaunti za mitandao ya kijamii ya TTB.  

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV