Kinachofuata baada ya kirusi kipya cha Corona
- Inashauriwa kuendelea kutoa taarifa za ugonjwa huo kwa mamlaka za afya.
- Watanzania wanashauriwa kuendelea kuchukua tahadhari.
Dar es Salaam. Endapo wewe ni mfuatiliaji mzuri wa habari, utakuwa umeshasikia juu ya aina mpya ya kirusi cha corona kilichogundulika nchini Afrika Kusini.
Kirusi hicho kilichopewa jina la Omicron kimeripotiwa kwa mara ya kwanza Novemba 24 katika nchi hiyo, miezi kadhaa baada ya kirusi cha Delta kutangazwa kutoka nchi hiyo hiyo.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kirusi hicho kinasambaa kwa haraka hivyo kinaweza kuwa na madhara makubwa kwa binadamu.
WHO imeshauri mamlaka za afya katika nchi mbalimbali kuchukua hatua za haraka dhidi ya Omicron ikiwemo kutoa taarifa juu ya ripoti za maambukizi zinazohusiana na kirusi hicho huku wananchi wakitakiwa kuendelea kuchukua tahadhari zote.
Latest
