Simu za rununu bado zipo zipo Tanzania

February 1, 2025 11:41 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ueneaji wa vifaa hivyo umeongezeka kwa asilimia 2.8 ndani ya kipindi cha miezi mitatu iliyopita.

Arusha. Matumizi ya intaneti yamezidi kushika kasi nchini yakichangia kuongezeka kwa watumiaji wa simu janja zinazowawezesha kuperuzi katika mitandao ya kurasa mbalimbali.

Licha ya kukithiri kwa matumizi ya simu hizo takwimu mpya za mawasiliano zinazotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zinabainisha kuwa idadi kubwa ya Watanzania bado wanatumia simu za rununu maarufu kama ‘viswaswadu’.

Takwimu hizo za robo ya mwaka unaoishia Disemba 2024 zinabainisha ueneaji wa simu za rununu umefikia asilimia 87.39 ambapo jumla ya vifaa milioni 56.8 vimeunganisha na mtandao.

Kwa mujibu wa TCRA ueneaji wa vifaa hivyo umeongezeka kwa asilimia 2.8 kutoka asilimia 84.8 iliyorekodiwa katika robo ya mwaka unaoishia Septemba 2024.

Wakati matumizi hayo ya simu za rununu yakiongezeka matumizi ya simu janja nayo yameongezeka mpaka asilimia 35.9 kutoka asilimia 33.8.

Hiyo ni sawa na kusema idadi ya vifaa vya simu janja vilivyounganishwa na mtandao hadi kufikia Disemba ni milioni 23.4.



1 thought on “Simu za rununu bado zipo zipo Tanzania

Comments are closed.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

🔴LIVE: WABUNGE WAKIJADILI HOTUBA YA WIZARA YA NISHATI BUNGENI

🔴LIVE: WABUNGE WAKIJADILI HOTUBA YA WIZARA YA NISHATI BUNGENI

Nukta TV

Kupigwa risasi: Sababu vifo 197 katika matukio ya ghasia Oktoba 29

Kupigwa risasi: Sababu vifo 197 katika matukio ya ghasia Oktoba 29

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.