Simu za rununu bado zipo zipo Tanzania

February 1, 2025 11:41 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ueneaji wa vifaa hivyo umeongezeka kwa asilimia 2.8 ndani ya kipindi cha miezi mitatu iliyopita.

Arusha. Matumizi ya intaneti yamezidi kushika kasi nchini yakichangia kuongezeka kwa watumiaji wa simu janja zinazowawezesha kuperuzi katika mitandao ya kurasa mbalimbali.

Licha ya kukithiri kwa matumizi ya simu hizo takwimu mpya za mawasiliano zinazotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zinabainisha kuwa idadi kubwa ya Watanzania bado wanatumia simu za rununu maarufu kama ‘viswaswadu’.

Takwimu hizo za robo ya mwaka unaoishia Disemba 2024 zinabainisha ueneaji wa simu za rununu umefikia asilimia 87.39 ambapo jumla ya vifaa milioni 56.8 vimeunganisha na mtandao.

Kwa mujibu wa TCRA ueneaji wa vifaa hivyo umeongezeka kwa asilimia 2.8 kutoka asilimia 84.8 iliyorekodiwa katika robo ya mwaka unaoishia Septemba 2024.

Wakati matumizi hayo ya simu za rununu yakiongezeka matumizi ya simu janja nayo yameongezeka mpaka asilimia 35.9 kutoka asilimia 33.8.

Hiyo ni sawa na kusema idadi ya vifaa vya simu janja vilivyounganishwa na mtandao hadi kufikia Disemba ni milioni 23.4.



1 thought on “Simu za rununu bado zipo zipo Tanzania

Comments are closed.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV