Sekta ya ajira ni mwendo wa kinyonga 2022 – Ripoti

January 18, 2022 9:22 am · Wilson
Share
Tweet
Copy Link
  • Corona yachangia kupotea ajira za watu wengi duniani.
  • Ukosefu wa ajira unakadiriwa kufikia wa milioni 207 mwaka huu.
  • Uboreshaji wa sera na mikakati ya ajira inaweza kutoa suluhu. 

Dar es Salaam. Shirika la Kazi Duniani (ILO) limeonya kuwa mwaka 2022 sekta ya ajira inatarajiwa kukua taratibu na tena bila uhakika kutokana na kuendelea kuwepo kwa janga la Uviko-19 ambalo limeathiri soko la nguvukazi ulimwenguni.

Ripoti mpya ya Ajira Duniani na Mtazamo wa Kijamii (WESO) iliyotolewa na ILO kuhusu mtazamo wa ajira duniani, inaeleza kuwa kuibuka kwa aina mpya vya virusi vya Uviko-19 ikiwemo  Delta na Omicron ni chanzo cha kupungua kwa ajira.

“Mtazamo wa soko la ajira duniani umezorota tangu makadirio ya mwisho ya ILO; kurudi kwa utendaji wa kabla ya janga ni uwezekano wa kubaki kuwa ngumu kwa sehemu kubwa ya ulimwengu katika siku zijazo,” inasomeka sehemu ya ripoti hiyo.

Ripoti hiyo imebainisha kuwa kuna uwezekano wa kuwepo kwa athari katika utofauti  baina ya makundi ya wafanyakazi na nchi na pengine zinaweza kuzidisha kukosekana kwa usawa baina ya nchi na nchi na hivyo kudhoofisha hali ya kiuchumi.

Ukosefu wa ajira duniani unatarajiwa kufikia watu milioni 205 katika 2022, na kupita kwa kiasi kikubwa kiwango cha milioni 187 cha mwaka 2019. 

Hii inalingana na kiwango cha ukosefu wa ajira cha asilimia 5.7. Ukiondoa kipindi cha mzozo wa Uviko-19, kiwango kama hicho kilionekana mara ya mwisho mnamo 2013.

Aidha ripoti hiyo imesema kuimarika na kurejea kwa hali ya kawaida  hutofautiana kwa kiasi kikubwa katika maeneo, nchi na sekta huku mwelekeo wa ukuaji katika nchi za kipato cha chini na cha kati umebaki kwa kiasi kikubwa chini ya zile zinazozingatiwa katika uchumi tajiri.


Zinazohusiana


Viashiria muhimu vya soko la ajira katika kanda zote – Afrika, Amerika, Nchi za Kiarabu, Asia na Pasifiki, na Ulaya na Asia ya Kati bado havijarudi katika viwango vyake kama ilivyokuwa kabla ya janga. 

“Bila juhudi za makusudi za kuharakisha uundaji wa nafasi za kazi zenye heshima, na kusaidia watu walio hatarini zaidi katika jamii na urejeshaji wa sekta zilizoathiriwa zaidi za kiuchumi, athari zinazoendelea za janga hili zinaweza kuwa nasi kwa miaka mingi kama wanadamu waliopoteza uwezo wa kiuchumi, umaskini mkubwa na ukosefu wa usawa,” amesema Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Guy Ryder. 

“Tunahitaji mkakati wa kina na ulioratibiwa, unaozingatia sera zinazozingatia binadamu, na kuungwa mkono na hatua na ufadhili. Hakuwezi kuwa na ahueni ya kweli bila kurejesha kazi zenye staha.”


Mapendekezo kuimarisha ajira

Pamoja na kuangalia saa za kazi na upotevu wa moja kwa moja wa ajira, na ukuaji wa kazi uliotabiriwa, WESO inaelezea mkakati wa uokoaji ulioandaliwa kulingana na kanuni nne: kukuza ukuaji wa uchumi mpana na uundaji wa ajira zenye tija; na kusaidia mapato ya kaya na mabadiliko ya soko la ajira.

Pia kuimarisha misingi ya kitaasisi inayohitajika kwa ukuaji na maendeleo shirikishi, endelevu na dhabiti; na kutumia mazungumzo ya kijamii kukuza mikakati ya uokoaji inayozingatia binadamu.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV