Sababu za Raha kuangazia wafanyabiashara huduma ya data Tanzania

May 24, 2021 8:58 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni huduma  ya ‘Azure Stack’ inayowezesha kutunza data za biashara katika teknolojia ya “cloud”. 
  • Pia ni njia rahisi ya kusambaza data ukiwa mtandaoni.

Dar es Salaam. Wafanyabiashara waliokuwa wakihaha kupata jukwaa bora la kutunza kumbukumbu na data za shughuli zao, wameendelea kupata suluhu baada ya Kampuni inayotoa huduma ya intaneti nchini Tanzania ya Raha kuzindua huduma  ya ‘Azure Stack’ ili kuongeza kiwango cha usalama mtandaoni. 

Huduma hiyo inayotolewa kupitia teknolojia ya “cloud” inawezesha biashara mbalimbali kupata jukwaa la kidijitali la kuhifadhi na kusambaza taarifa au data za shughuli zao za kila siku huku wakijihakikishia usalama na usiri wa taarifa zao.

Jukwaa hilo huenda likawafaa zaidi vijana wanaomiliki kampuni na biashara zinazochipukia kupata eneo sahihi kutunza data kwa ajili ya kufuatilia mwenendo wa shughuli zao na huduma wanazotoa kwenye jamii. 

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Raha Limited nchini Tanzania, Reuben Lucas amesema kuzinduliwa kwa huduma hiyo ni kukidhi ukuaji wa mahitaji ya biashara kutafuta majukwaa salama ya mtandaoni ambako wanaweza kuhifadhi data zao.

Amesema kwa sasa, kampuni nyingi zinaendesha shughuli zao mtandaoni na uanzishwaji wa mifumo thabiti ya kidijitali ni muhimu kuwahakikisha biashara hizo zinakuwa endelevu na zinachangia katika maendeleo ya Taifa. 

“Usambazaji wa huduma hii ya ‘Azure Stack’ nchini ni hatua nyingine kubwa tuliyoifanikisha huku tukiendelea kusaidia kuhamasisha maendeleo thabiti ya kiuchumi na kiteknolojia tunayoyaona kuwahi kutokea Tanzania hapo awali,” amesema Lucas katika uzinduzi wa huduma hiyo uliofanyika Mei 20 jijini Dar es Salaam.


Zinazohusiana


Ili kupata huduma hiyo ambayo kwa sasa inapatikana katika miji 60  duniani, mteja anatakiwa kuwasilisha taarifa na kulipia kulingana na mahitaji yake na kisha utaunganishwa bila kuhitaji kuweka miundombinu katika biashara yake.

Huduma hiyo haiitaji mfanyabiashara kununua vifaa vya kuhifadhia data kama kanzidata (servers) na huduma zinazohusiana jambo linalopunguza matumizi katika kampuni hasa zinazochipukia.

Pia inapunguza changamoto ya usafirishaji wa data na inawezesha shughuli za kibiashara kuendelea kufanyika kwa ufanisi kutokana na mifumo iliyowezeshwa kuendana na mabadiliko ya kimazingira.

“Sasa, wateja wetu katika ukanda wote wa Afrika ya Mashariki wana uhakika wa mazingira salama na ya kuaminika kwenye shughuli zao za Tehama muda wowote,”-  amesema Afisa Mtendaji Mkuu wa Liquid Telecom, ambayo ni kampuni mama ya Raha Limited,  Adil El Youssefi.

Raha inahudumia biashara zaidi ya 1,500 kwa kuwaunganisha na huduma ya intaneti ili kurahisisha utendaji wa shughuli zao nchini.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴 LIVE: WABUNGE WAKIMCHAPA MASWALI MAZITO WAZIRI MKUU BUNGENI

🔴 LIVE: WABUNGE WAKIMCHAPA MASWALI MAZITO WAZIRI MKUU BUNGENI

Nukta TV

CEO, TAB Group: Africa Agri Expo 2026 inakwenda kufungua fursa kimataifa, kilimo cha Tanzania

CEO, TAB Group: Africa Agri Expo 2026 inakwenda kufungua fursa kimataifa, kilimo cha Tanzania

Nukta TV

TANTRADE: Tumieni vifungashio vya "Made in Tanzania"

TANTRADE: Tumieni vifungashio vya "Made in Tanzania"

Nukta TV