Riba, viwango vya kubadili fedha, sababu madeni ya nchi za Afrika kukua kwa kasi

March 7, 2024 1:18 pm · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Awali ukuaji wa madeni ulikuwa unaendana na ukopaji tofauti na sasa.
  • Nchi za Afrika zakutana kutafuta mwarobaini.

Dar es Salaam. Imeelezwa kuwa kuongezeka kwa viwango vya riba pamoja na viwango vya kubadilisha fedha duniani, ndio chanzo cha kushuka kwa thamani ya fedha za nchi za Afrika pamoja na kukua kwa kasi kwa madeni ya nchi hizo.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Elijah Mwandumbya, aliyekuwa akizungumza wakati wa mkutano wa 56 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi kutoka nchi za Umoja wa Afrika amesema awali ukuaji wa deni ulikuwa unaendana na ukopaji lakini kwa sasa imebainika kuwa kuna sababu zingine zinazochochea kuongezeka kwa deni hilo.

“Sababu hizo ni pamoja na mabadiliko makubwa ya viwango vya kubadilisha fedha na riba hivyo kuzifanya nchi za Afrika kutafuta njia mbadala ya kutatua changamoto hiyo,” amesema Mwandumbya aliyemuwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba jijini Victoria Falls, nchini Zimbabwe.

Mwandumbya ameongeza kuwa katika kulihudumia deni “dept service” lililoongezeka, kumekuwa na changamoto kubwa kwa sababu nchi nyingi bado hazina uwezo wa kukusanya mapato ya kutosha kugharamia huduma mbalimbali.


Soma zaidi: Serikali yajipanga kuongeza viwango vya ukusanyaji kodi Tanzania


Aidha, Mwandumbya amebainisha kuwa, katika kukabiliana na changamoto za ukuaji wa madeni hususani kipindi hiki cha mabadiliko makubwa ya tabianchi ni muhimu kwa nchi za Afrika kuwa na mkakati wa kuhakikisha zinapata rasilimali fedha ili mipango inayotekelezwa iweze kukidhi mategemeo ya wananchi.

“Changamoto kubwa ambayo tunaiona hapa kwa nchi zetu za Afrika ni ile haja ya kuendelea kukusanya mapato ya kutosha ili kujihakikishia kwamba tunaweza kupata rasilimali za kuweza kuhudumia deni lakini pia tunaweza kulipa mishahara pia kuhudumia gharama mbalimbali za kibajeti,” ameongeza Mwandumbya.

Kwa mujibu wa Mwandumbya, miongoni mwa ajenda kubwa zinazojadiliwa katika mkutano huo ni kupata suluhu ya namna gani nchi zitaboresha viwango vya ukusanyaji wa mapato ili kutoka kwenye viwango vya chini ya asilimia 11 na 12 ya ukuaji wa mapato ya ndani (GDP) kwenda viwango ambavyo vinavyokubalika kuanzia asilimia 16.

Itakumbukwa Mwezi Februari, Makamu wa Rais wa Tanzania Dk. Philip Mpango alibanisha kuwa Serikali ipo mbioni kutafuta suluhu itakayoongeza viwango vya ukusanyaji wa kodi hadi kufikia asilimia 15 ya pato la Taifa ili kuwezesha shughuli za maendeleo na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Mkutano huo wa 56 unaratibiwa na Uneca, jukwaa lililoanzishwa na Umoja wa Mataifa ili kuzisaidia nchi za Afrika kufanya mijadala na tafiti mbalimbali ili kuzalisha na kufanya ubunifu utakaokuza uchumi hivyo kutengeneza fursa ya kujadiliana na kuhakikisha ushauri unaotolewa unaendana na mazingira halisi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV