Rais Samia : Simamieni haki kuimarisha imani ya mahakama Tanzania

September 14, 2023 12:35 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Asisitiza kufanya kazi kwa maadili kuchochea upatikanaji wa haki
  • Mahakimu, majaji wasio waadilifu kuchukuliwa hatua

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amewataka majaji kusimamia haki ili kujenga imani ya mahakama kwa wananchi na kuongeza ufanisi katika shughuli za mhimili huo muhimu.

Rais Samia aliyekuwa akizungumza leo Septemba 14, 2023 wakati akiwaapisha viongozi aliowateua Ikulu jijini Dar es Salaam, amebainisha kuwa wateule hao watasaidia kupunguza mlundikano wa kesi na kuongeza ufanisi katika shughuli za mahakama.

“Ni imani yetu kuwa mlioteuliwa mtaenda kufanya kazi kwa jitihada zote ili mabadilko tunayozungumza tukayaone…tunaomba muongeze nguvu ili mkafanye vizuri na haki ipatikane mapema,” amesema Rais Samia.


Soma zaidi


Viongozi walioapa leo ni pamoja na majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu, ikiwa ni sehemu ya  utekelezaji wa mapendekezo ya tume ya haki jinai iliyoshauri kuimarisha uwezo wa mahakama katika teknolojia, kuboresha majengo na rasilimali watu.

Tangu Rais Samia aingie madarakani mwezi Machi mwaka 2021, ameteua majaji wa mahakama kuu 63, na kufanya Tanzania iwe na jumla ya majaji 105, idadi  inayotajwa kuiweka Tanzania kwenye nafasi nzuri ya kutoa haki kwa wananchi.

Wasio na nidhamu watahadharishwa

Kufuatia kuwepo kwa vitendo vya uvunjifu wa maadili unaofanywa na majaji na mahakimu katika mahakama, Serikali kupitia Mahakama Kuu imeanzisha tume inayyochunguza mwenendo wa maadili ya viongozi hao.

Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma amebainisha kuwa kuanzia mwaka mwaka 2015 hadi 2019 jumla ya mashauri 99 ya uvunjifu wa maadili yalikusanywa ambapo 33 kati yao walifukuzwa kazi huku 38 wakistaafishwa.

“Waliofukuzwa kazi  na kustaafishwa ni asilimia 71…kwa hiyo majaji msiingie katika anga ya tume katika masuala ya nidhamu,” amesema Profesa Juma.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: LIVE:WABUNGE WAKIWACHAPA MASWALI MAWAZIRI | Bunge la 13 | Kikao cha 28

🔴LIVE: LIVE:WABUNGE WAKIWACHAPA MASWALI MAWAZIRI | Bunge la 13 | Kikao cha 28

Nukta TV

Top 10 ya magari yanayotumia kiwango kidogo cha mafuta

Top 10 ya magari yanayotumia kiwango kidogo cha mafuta

Nukta TV

SGR yaingizia Serikali Sh169.37 bilioni tangu kuanza kwa safari Juni 2024

SGR yaingizia Serikali Sh169.37 bilioni tangu kuanza kwa safari Juni 2024

Nukta TV